ULAYA LEO:- MAGAZETI NA TETESI ZA UAMISHO WA WACHEZAJI(ARSENAL - ESSIEN, CHELSEA - SCHURRLE NA TIMU ZINGINE - PERUZI)

FLETCTHER KUCHEZA ULAYA

Kiungo wa Manchester United, Darren Fletcher anatarajiwa kutajwa kwenye kikosi cha Ligi ya Mabingwa cha United, licha ya kwamba hajacheza mechi yoyote ya ushindani tangu Novemba.

Dimitar Berbatov, mwenye umri wa miaka 31, sasa anafanya kila liwezekanalo kuhakikisha anakamilisha uhamisho wake kwenda Fulham kutoka Manchester United.


Beki wa Tottenham na England, Michael Dawson, mwenye umri wa miaka 28, anaweza kuondoka tu White Hart Lane, licha ya kwamba majeruhi ya Younes Kaboul yanaweza kumuweka nje ya uwanja hadi Krisimasi.
Arsenal inataka kufanya usajili wa ghafla na wa kushitua wa kiungo wa Chelsea, Michael Essien. Arsene Wenger anamtaka kiungo huyo mwenye umri wa miaka 29 kwa mkopo baada ya mambo yake kumuendea kombo Stamford Bridge.
Mshambuliaji wa Arsenal, Nicklas Bendtner, mwenye umri wa miaka 24, amepewa ofa na Stoke City ya kusajiliwa kwa mkopo, lakini klabu nyingine kadhaa zinawasiliana na mwakilishi wake.
Chelsea inajiandaa kumtoa kwa mkopo mshambuliaji Daniel Sturridge, mwenye umri wa miaka 22, kama watafanikiwa kukamilisha usajili wa mchezaji wa Bayer Leverkusen, Andre Schurrle. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 anaweza kugharimu pauni Milioni 20.

Post a Comment

Previous Post Next Post