HII NDIO AJALI ILIYOTOKEA ENEO LA FERI JIJINI DAR ES SALAAM


Mkazi wa jijini Dar akiwa amegongwa na daladala eneo la Feri jioni hii

Hapa bajaji iliyombeba majeruhi ikipita karibu na daladala iliyomgonga mkazi huyo

Huyu ni dereva wa daladala iliyomgonga mkazi huyo akijiandaa kukimbia kabla ya kukamatwa
Majeruhi aliyegongwa na daladala jioni hii

Hapa akiwa katika usafiri wa Bajaji tayari kukimbizwa Hospitali
mkazi mmoja wa jijini Dar es Salaam ambaye jina halijaweza patikana mara moja amenusurika kifo baada ya kugongwa na daladala yenye namba za usajili T710 ALV linalofanya safari zake kati ya Posta na Mwananyamala .

Ajali hiyo imetokea majira ya saa 11.30 jioni wakati mkazi huyo akijaribu kuvuka barabara kutoka eneo la Mahakama kuu kuelekea kituo cha polisi cha Askari wa wanamaji ufukweni wa bahari ya Hindi.

Askari wa kikosi cha usalama barabarani wamefika eneo la tukio na kumchukua majeruhi huyo kwa usafiri wa Bajaji na kumpeleka Hospitali kwa matibabu zaidi huku dereva wa Daladala hilo akikamatwa

Post a Comment

Previous Post Next Post