KWELI KUNDI LA KLABU BINGWA ULAYA TULILOPO NI GUMU(MAN CITY,BORUSSIA DORTMUND NA AJAX AMSTERDAM) - MOURINHO

Jose Mourinho

   MADRID, Hispania

KOCHA Jose Mourinho wa Real Madrid amekiri hatimaye kwamba bklabu yake imepangwa kwenye kundi gumu katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. 

Manchester City wataanza kuivaa Real Madrid kwenye Uwanja wa Bernabeu Septemba 18, huku mabingwa wa Bundesliga, Ligi Kuu ya Ujerumani, Borussia Dortmund na mabingwa wa Ligi Kuu ya Uholanzi, Ajax, pia wakiwa katika kundi hilo la D. 

Mourinho amesistiza kwamba wachezaji wake hawatakuwa tayari kufanya makosa yoyote yale katika mechi zao sita ngumu za kundi hilo kama watataka kujihakikishia nafasi ya kufuzu kwa hatua ya 16-bora. 

Ameiambia AS: "Sio tu kwamba kuna mabingwa wa Ligi Kuu nne, bali ni mabingwa wa ligi kuu tatu kali zaidi barani Ulaya -- zaLa Liga (Hispania), Ligi Kuu ya England na Bundesliga. 

"Kwangu mimi naona kama soka la Italia limeyumba kiasi.
"Soka la Ufaransa ni wazi kwamba linaimarika, lakini bado halijafikia kiwango chetu. 
"Ni kundi gumu sana. 

"Na nyingine inayokamilisha kundi hili ni Ajax, ambao kila mara huwa na kazi ya kujenga upya kikosi chao lakini siku zote huonekana kuwa wazuri katika kupata wachezaji wapya wakali, vijana ambao hulenga kujitengenezea majina na kupambana kwa lengo hilo."

Post a Comment

Previous Post Next Post