Tottenham iko tayari kumto kwa mkopo kiungo wa England, Jermaine Jenas,
mwenye umri wa miaka 29, akacheze Daraja la Kwanza ili kujihakikishia
nafasi ya kucheza mechi.
Hull City na Huddersfield zote zina nia ya kumsajili
mshambuliaji wa Sunderland, Fraizer Campbell kwa mkopo. Mchezaji huyo
mwenye umri wa miaka 24 alipandishwa kucheza Ligi Kuu akicheza kwa mkopo
Hull mwaka 2008.
Stefan Oakes, mwenye umri wa miaka 33, kiungo ambaye alishinda Kombe la
Ligi akiwa na Leicester City na kucheza mechi zaidi ya 60 za Ligi Kuu,
anaweza kutimkia Spalding United, ambayo inachesa Ligi Kuu ya United
Counties.
Mshambuliaji Nicklas Bendtner, mwenye umri wa miaka 24, ambaye
amesajiliwa Juventus kwa mkopo wa msimu wa muda mrefu kutoka Arsenal
wiki iliyopita, ameambiwa hayuko katika hali nzuri kimchezo ya kuchezea
Kibibi Kizee hicho cha Turin.
Mshambuliaji wa Manchester United, Josh King, mwenye umri wa miaka 20,
ameionya klabu hiyo kwamba yupo tayari kuondoka Januari kama hatapata
nafasi ya kucheza japo mechi kadhaa.
Zenit St Petersburg inatumai kukamilisha usajili wa pauni
Milioni 25 wa winga wa Manchester United, Nani, mwenye umri wa miaka 25,
kabla ya kufungwa pazia la usajili la Urusi leo.
Post a Comment