PETER MSECHU NDANI YA MAREKANI


Mwaka huu umekuwa wenye baraka tele katika nchi yetu ya Tanzania kwani mara ya kwanza tumeona Diamond Platinum juzi juzi  tu alikuwa ndani ya Washington Dc nchini marekani kwa kupiga show yake,mara ya pili tukaona Martin Kadinda ambaye anahusika na mambo ya fashion designer alipata mwaliko Neywork city.Sasa habari nzuri ni kwamba Peter msechu naye ndani ya Chicago.Msanii huyu alifunguka na kusema kwamba yeye ameenda kwa kupiga show kadhaa pamoja na vitu vyake binafsi kwani msanii huyu ana mchakato wa kufunguka band yake kwa hiyo huku ameenda kwa kuulizia bei ya vifaa ambavyo ataweza kufungulia band yake.Pia alisema kwamba atakaa kama miezi 6 nchini humu mpaka mambo yake yakamilike ndipo atarudi nchini Tanzania.
              Hii ni moja kati ya picha ambayo msanii huyu alipiga akiwa katika maeneo ya Downtown Chicago.
                          Peter Msechu akiwa na rafiki yake katika maeneo ya millenium park chicago.

Post a Comment

Previous Post Next Post