Kenya kuzuia hotuba za chuki wakati uchaguzi unakaribia

Katibu Mkuu wa Baraza la maimamu na Wahubiri wa Kenya Sheikh Mohamed Dor akifikishwa katika mahakama ya Mombasa hapo tarehe 18 Oktoba ambako alishitakiwa kwa kuchochea vurugu. [Na AFP]
Na Rajab Ramah, Nairobi

Serikali ya Kenya imeweka miongozo mikali ya kikemea hatuba za chuki wakati nchi inajitayarisha kufanya uchaguzi mkuu mwezi Machi.

Sheria hizo mpya, zinazoitwa "Miongozo ya Kuzuia Upelekaji wa Ujumbe wa Siasa Usiotakiwa kupitia Mitandao ya Mawasiliano ya Elektroniki", zilitangazwa mjini Nairobi siku ya Jumatano (tarehe 24 Oktoba).

Miongozo hiyo itasimamia ujumbe zinazotumwa kupitia simu za mikononi pamoja na usambazaji wake katika mitandao ya kijamii ili kuhakikisha hakuna ujumbe za kuchokoza au kushawishi unatumwa katika Twitter au Facebook, alisema Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari na Mawasiliano Bitange Ndemo.

Miongozo hiyo inawataka wanasiasa kupeleka maandiko ya ujumbe wa kampeni zao na matangazo ya kisiasa kwa ajili ya kuchunguzwa angalau siku mbili kabla haijatumwa, kusemwa au kutangazwa kwa umma.

Tume ya Taifa ya Maelewano na Maingiliano, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka, Tume ya Mawasiliano ya Kenya (CCK), polisi na sekta nzima ya mawasiliano ya simu, ambazo zilitoa miongozo hiyo, zitasaidia ili kuimarisha miuongozo hiyo, Ndemo alisema.

"Wale watakaokiuka kanuni hizi watapelekwa jela," Ndemo aliiambia Sabahi. Alisema kuwa mtu yeyote atakayetuma ujumbe za kutishia, kutukana, kunyanyasa na ujumbe za uchochezi zenye uwezo kuchochea chuki za kikabila kwa kutumia simu za mikononi na wale wanaovunja sheria za kisiasa watakabiliwa na adhabu ya faini ya shilingi milioni 1 (dola 11,700), muda wa jela hadi miaka mitatu, au yote mawili.


Ndemo alisema miongozo hiyo imekusudia kuzuia vurugu ambazo ziliikumba nchi baada ya uchaguzi wa raisi wa mwaka 2007.

Wanasiasa wakuu walishitakiwa kwa kuchochea vurugu katika uchaguzi wa mwaka 2007, ambao ulisababisha vifo vya watu wanaokisiwa 1,200 na zaidi ya watu 300,000 kukimbia makazi yao, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.

"Kwa mujibu wa ripoti za kiintelijensia, vurugu za kisiasa ambazo zilizikumba sehemu nyingi nchini mwaka 2007 na mwanzoni mwa mwaka 2008 kwa kiasi kikubwa zilisababishwa na matumizi ya lugha isiyokuwa ya kuwajibika na ya uchochezi wakati wa kugombea na mara tu baada ya uchaguzi," Ndemo alisema. "Ili kutumia vizuri jukwaa la simu za mikononi na kuimarisha utamaduni wa kidemokrasia na kuzuia umwagaji damu, imekuwa ni jambo la haraka kuweka kanuni hizi ili kulinda dhidi ya usambazaji wa ujumbe za chuki."

Ndemo alisema kuwa utekelezaji wake utafanywa kuwa rahisi zaidi mwezi ujao ambapo simu zote za mikononi zitaandikishwa na serikali.

"Miongozo hiyo pia inawataka wafadhiliwa wa ujumbe za kisiasa sio tu kujitambulisha wenyewe bali pia kutia saini nyaraka zinazowaidhinisha kutuma ujumbe hizo na kuhakikisha wajibu wao unafuata kanuni," Mkurugenzi wa CCK Francis Wangusi aliiambia Sabahi.

Miongozo hiyo pia itataka ujumbe wa maandshi uweze kutumwa tu baina ya saa mbili asubuhi hadi saa 12 jioni, zikiwa zimetumika lugha za Kiingereza na Kiswahili tu na sio katika lugha nyingine zozote zinazotumiwa na jamii za makabila.

Mary Ombara, mjumbe wa Kamati Elekezi ya Taifa juu ya Usomaizi wa Vyombo vya Habari, alisema kuwa miongozo hiyo inavitaka vyombo vyote vya habari kuwatumia waandishi wa habari wataalamu tu katika kuendesha majadiliano ya kisiasa au kuandika maoni juu ya matukio ya kisiasa nchini.

Aliiambia Sabahi kuwa waandishi wa habari wataalamu wana kiwango kikubwa cha busara na uwajibikaji na hii itazuia ripoti juu ya matamshi ya uchochezi kutoka kwa wanasiasa. "Tutakuwa tukisimamia kwa makubaliano," alisema. "Hatutaki tukamatwe tukiwa hatukujitayarisha."

Post a Comment

Previous Post Next Post