Mwanasheria mkuu wa serikali ya Kenya atangaza kadi ya kurekodia ya mahakama

Na Rajab Ramah Nairobi

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Kenya Willy Mutunga alitangaza kadi ya kurekodia ya mahakama ambayo ndiyo kwanza imeanzishwa kwa mara ya kwanza katika jengo la Mahakama ya juu jijini Nairobi Ijumaa (tarehe 19 Oktoba).

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Kenya Willy Mutunga alitangaza tarehe 19 Oktoba Hali ya Ripoti ya Mahakama ikijumuisha mwaka wake mmoja aliyekaa ofisini. [File photo]

Hali ya Ripoti ya Mahakama huchukua muda wa mafanikio ya mahakama na changamoto ambazo taasisi hiyo imekutana nazo katika kusimamia haki kwa mwaka uliopita.

Mutunga alisema mwaka uliopita mahakama ilirekodi maendeleo makubwa mno, ikikamilisha kesi 421,827 kati ya 428,827 zilizofunguliwa kati ya Juni 2011 na Juni 2012.

Alisema mahakama ilikodi wafanyakazi waandamizi 251, ilianzisha mahakama kuu nne mpya, ilianzisha mahakama mbili za kati na ilizindua mahakama jongezi kwa ajili ya maeneo ya mbali na maeneo yaliyoachwa.

"Kwa kipindi ambacho kinatathminiwa, uwiano wa hakimu kwa watu ulikuwa jaji mmoja kwa Wakenya 500,000 na hakimu mmoja kwa 90,000," Mutunga alisema. "Kutoka katika hali tata kama hiyo, inashangaza kidogo kwamba moja ya hati ya kushtaki ya kawaida ya mahakama imekuwa ikishindwa kutoa haki pasipo kuchelewesha. Kwa sababu yoyote itakayotolewa ya ucheleweshaji katika siku zilizopita, katiba sasa inataka haki isicheleweshwe."

Kuondoa ucheleweshaji na kuondoa viporo vya kesi, mahakama itaongeza teknolojia kusaidia uainishaji wa kesi kwa kusikiliza na kutoa hukumu haraka, Mutunga alisema, akiongezea kuwa mahakama pia inatarajia kuanzisha angalao mahakama moja kubwa katika wilaya zote 47 kwa kipindi cha miaka kumi ijayo na kukodi mahakimu zaidi 147 kuondoa tatizo la uhaba wa wafanyakazi.

"Hakimu ni zao la watendaji wanaofanya kazi hatua kwa hatua kwa kushirikiana katika kufikia lengo moja," alisema. "Mahakama ni moja ya mambo kama hayo -- watendaji wengine ni pamoja na Kurugenzi ya Kesi za Wananchi, polisi, magereza, mwanasheria mkuu, wizara kadhaa na asasi za kijamii.

"Ili mfumo wa mahakama uweze kufanya kazi kwa ufanisi, ushirikiano wa pamoja wa ulinganifu na wajibu wa kukamilishana ni muhimu," alisema.

Mutunga alisema kwa miaka iliyopita, mahakama zilianzisha sheria zilizorahisishwa, kukamilisha ujenzi wa jengo la mahakama lililokuwa limesimama, kuanzisha utambuzi wa umma kuhusu upatikanaji wa mahakama, kuhuisha Fedha za Mahakama ili kukamilisha gharama za kiutawala na kuanzisha mfumo wa malalamiko ya umma.

Makamu wa Rais Kalonzo Musyoka, aliyemwakilisha Rais Mwai Kibaki katika sherehe za utoaji wa ripoti hiyo siku ya Ijumaa, aliisifu mahakama kwa "mabadiliko yake makubwa na maendeleo" kwa mwaka uliopita.

"Tumepitia njia ndefu kama taifa huru na leo watu wa kawaida katika mitaa ya jiji na majiji mengine wanayaona mabadiliko haya kwa uwazi na mabadiliko haya yaliyokuja na yanaendelea kuja kwetu," alisema.

Mwenyekiti wa Shirika la Kisheria Eric Mutua aliiambia Sabahi ripoti itaongeza ushiriki wa umma katika mahakama na kwamba huduma zilizoboreshwa zitarejesha ujasiri wa umma katika mahakama.

Otiende Amollo, mwenyekiti wa Tume ya Utawala wa Mahakama, alisema tume imeridhishwa na utendaji wa mahakama. Alisema ripoti ya mwanasheria mkuu ilionyesha wajibu wa mahakama katika jamii.

"Hii ni njia moja ya kufungua mahakama na kuwafanya watu waziamini zaidi mahakama, wakiepuka matukio ambayo jamii inajichukulia sheria mikononi mwao kwasababu wanaona utekelezaji wa sheria unafanyika taratibu na wakati mwingine hautendi haki," Amollo aliiambia Sabahi.

Alisema mahakama ni mkono pekee wa serikali ambao umeachwa katika matarajio ya umma na mahitaji ya katiba kuwasilisha ukaguzi wa mwaka.

Ili kulinda faida zilizopatikana katika mabadiliko ya mahakama, Amollo alisema uteuzi wa maofisa wa mahakama unapaswa kuharakishwa ili kuepuka wasiwasi unaosababishwa na kuchelewa. Alitoa wito kwa asasi za kijamii kuwa watulivu na kukataa jitihada zozote za kunazopinga mabadiliko.

Post a Comment

Previous Post Next Post