Mwenyekiti wa bodi ya shirika la BBC Lord Patten, ametoa
hakikisho kuwa BBC itaendelea kuwa huru na haitaathiriwa na serikali
licha ya kashfa ya madai ya udhalilishaji watoto kimapenzi inayodaiwa
kutekelezwa na aliyekuwa mtangazaji nyota wa runinga, Jimmy Savile.
Bwana Lord Patten, alisema hayo akimjibu waziri wa maswala ya utamaduni Maria Miller ambaye alikuwa amesema kuwa tukio hilo limepunguza imani ya wananchi kwa BBC.
إرسال تعليق