
Baada ya miaka 35 ya utumishi wa uaminifu katika Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Ujerumani, Othmani Miraji ijumaa
hii, 12.10.2012, ilikuwa siku yake ya mwisho kazini kama mhariri
mwandamizi.Wafanyakazi wenzake, wakiongozwa na mhariri mkuu wa DW, Bibi
Ute Shaeffer, na pia mkuu wa matangazo ya Kiswahili, Bibi Andrea
Schmidt, walimfanyia karamu murua ya kumuaga na kumtakia kila la heri na
afya njema katika maisha yake ya baadae. Pia walisifu mchango mkubwa
alioutoa katika kuifanya DW iwe kuinganisho cha kupata habari za
kuaminika na mototo kutoka duniani kote na katika kuikuza lugha ya
Kiswahili. Othman Miraji alijiunga na DW akitokea idara ya kunasa
matangazo ya BBC Monitaring service, Nairobi, Kenya, mwaka 1977 ambako
alitumika kwa miaka saba.
إرسال تعليق