PENZI LA NEY WA MITEGO LAMCHANGANYA BINTI WA 20 PERCENT



Asfa Omary Neema
 MWIGIZAJI wa kike katika ya tasnia Bongo Movies Asfa Omary Neema 20% ameshindwa kuficha hisia zake pale alipodai kuwa pamoja na umri wake mdogo anamzimia sana msanii wa Bongo fleva, Ney wa Mitego.

 "Siyo siri ,nampenda sana Ney wa Mitego na natamani awe mume wangu wa ndoa hata kesho kama akikubali, kama ingekuwa wasichana tunaruhusiwa kuwatongoza wanaume na kuolewa nao basi mimi ningekuwa wa kwanza kwa Ney, ana mvuto na shababi"  Neema 20%.

Neema ni msanii aliyevuma na kuibuka kupitia filamu ya 'Furaha Iko Wapi' iliyotungwa na msanii wa muziki wa Bongo fleva Hamis Kinzasa "20 Percent" amedai kuwa anampenda mwanamume anayejiamini na kuwa mtanashati...

Anadai kuwa hizo sifa anaziona kwa  msanii Ney  pekee na si mtu mwingine, na atafanya kila juhudi ili aweze kuishi na msanii huyo

Post a Comment

Previous Post Next Post