KATIBU WA ZAMANI WA SIMBA HASANOO KORTIN KWA WIZI WA PEMBE ZA NDOVU


MWENYEKITI wa Chama cha Soka Pwani (Corefa), Hassani Othman maarufu kama Hasanoo (43) na wenzake watano wamefikishwa katika Mahakamaya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu, likiwemo la uhujumu uchumi na kusafirisha pembe za ndovu (Meno ya Tembo)   kutoka Dar es Salaam kwenda Hong Kong, yenye thamani ya Sh1.1 bilioni.
Wakili wa Serikali, Shedrack Kimaro jana aliwataja washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando kuwa ni Ally Kimwaga, Dastan Mwanga, Godfrey Mwanga, John Mlai na Khalid Fazaldin.
Kimaro alidai katika shtaka la kwanza kuwa, kati ya Septemba Mosi na Novemba 20, mwaka huu, Dar es Salaam na Hong Kong kinyume na kifungu cha 384 ya kanuni ya adhabu sura ya 16.
Amesema washtakiwa hao kwa pamoja walikula njama ya kujihusisha na biashara ya nyara za serikali bila ya kuwa na leseni inayowaruhusu kufanya hivyo.

Post a Comment

أحدث أقدم