Mkuu wa mkoa wa singida
Kikundi
cha nyota njema kikitumbuiza ngoma ya asili ya kabila la Kinyaturu
wakati wa maadhimisho ya siku ya kupinga vitendo vya ukatili wa
kijinsia
Na Elisante John;Singida
Novemba 28,2012.
SERIKALI
imeyataka mashirika ya kiraia kushirikiana pamoja, ili kupiga vita na
hatimaye kutokomeza kabisa vitendo vinavyosababisha ukatili wa kijinsia,
hususani wanavyofanyiwa wanawake na watoto wadogo nchini.
Hayo
yamebainishwa mjini Singida na mkuu wa mkoa huo, Dk. Parseko Kone,
kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake,
yaliyoadhimishwa kitaifa katika viwanja vya Peoples, mjini Singida,
jana.
Maadhimisho
hayo, yamefanyika mkoani Singida, kwa ushirikiano wa mashirika 16 hapa
nchini, yaliyoipa dhamana ya kusimamia sherehe hizo, shirika la Action
Aid-Singida,huku kauli mbiu yake ikiwa ‘FUNGUKA! Kemea ukatili dhidi ya
wanawake, sote tuwajibike’.
Dk.
Kone alisema kuwa, kutokana na changamoto nyingi zinazowakabili
wanawake ikiwemo ukatili wanaofanyiwa na wanaume, serikali kwa
kushirikiana na mashirika ya kirai bado yanayo kazi kubwa katika
kuungana pamoja ili kutokomeza unyanyasaji huo.
“Madhara
yatokanayo na ukatili kwa wanwake katika jamii hupunguza nguvu kazi ya
Taifa, baadhi ya madhara ya ukatili huo ni mauaji ya wanawake, ulemavu
wa kudumu wa viungo…kupungua kwa uzalishaji kwa kuwa mwanamke ndiye
mzalishaji mkuu kwenye kaya nyingi hapa nchini,”alisema Dk. Kone.
Mapema
akimkaribisha mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, mkuu wa wilaya
Singida mwalimu Queen Mlozi aliagiza kuwa ni vema sherehe kubwa kama
hiyo inapofanyika mkoani hapa, wahusika wakashirikisha serikali ili
iweze kufana zaidi.
Mwalimu
Mlozi alilazimika kutoa amri hiyo, baada ya maadalizi, husani hamasa
kuwa katika kiwango cha chini sana, hali iliyochangia uwanja kuonekana
mtupu kutokana na watu wachache sana kujitokeza, vikiwemo vikundi
vichache vya hamasa.
“Jamani
ni vizuri maadhimisho makubwa kama haya yanapoletwa mkoani kwetu, basi
wahusika wajitahidi kushirikisha serikali washirikiane pamoja
kuhamasisha wananchi ili wajitokeze kwa wingi na wafurike kwenye
sherehe,”alisema kwa masikitiko Mlozi.
Akizungumzia
maadhimisho hayo, Juliana Bwire, afisa usawa na jinsi wa shirika la
Concern worldwide kutoka jijini Dar es Salaam alisema siku 16 walizokuwa
Singida, walizitumia vijijini kuielimisha jamii madhara ya ukatili,
ikiwemo unyanyasaji, ukeketaji, na wanawake kunyimwa haki.
Aidha
mmoja wa wanawake waliohudhuria sherehe hizo, Happynes Juma(30) mzaliwa
wa Kigoma, alieleza kwa masikitiko ukatili aliofanyiwa na mumewe
ikiwemo kudaiwa hajui kufanya mapenzi, hali iliyoleta mgogoro wa
kifamilia na suala hilo lipo ustawi wa jamii, tayari kwa ajili ya
kutengana.
Alisema maadhimsho hayo yatahitimishwa jijini Dar es Salaam siku ya desemba 8, mwaka huu
Post a Comment