Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
(Watatu kulia, waliobeba jeneza) akishiriki kubeba jeneza lenye mwili wa
aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani
maarufu kwa jina la Sharo Milionea, alipokiwakilisha Chama Cha
Mapinduzi, kwenye mazishi ya msanii huyo, leo kwenye Kijiji cha
Lusanga, Muheza Tanga.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye
akitoa pole za Chama Cha Mapinduzi (CCM) alipokiwakilisha Chama Cha
Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi
kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo
Milionea,leo kwenye Kijiji cha Lusanga, Muheza Tanga
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nauye,
akitupa mchanga kaburini, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM)
kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu,
Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji
cha Lusanga, Muheza Tanga.
Mkuu wa wilaya ya Muheza, Subra Mgalu akisoma
salam za Shirika la Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) la Mama Anna Mkapa,
kwenye msiba huo. Pamoja naye ni Nape
(Picha na Bashir Nkoromo).
Post a Comment