MWANAMKE ALIYEJIFANYA MWANAMME KWA UUME BANDIA AUAWA

 
Mapenzi yalipokuwa motomoto.
 
Wakati wa ugomvi wao wa kila mara.
 
Elizabeth alivyo leo.

ELIZABETH Rudavsky wa nchini Canada  alimuua ‘mumewe’ Angelo Heddington mwaka 2003 wakati akijihami asiendelee kumshambulia.  Ni baada ya kumuua ndipo alipofahamu kwamba mtu ambaye alikuwa akijifanya mumewe kumbe alikuwa ni mwanamke aliyekuwa anatumia uume wa bandia.

Tukio hilo limeripotiwa na vyombo vya habari baada ya mlolongo wa mrefu wa mashitaka dhidi ya Elizabeth, 27,  ambaye alimchoma Angelo, 30,  (jina lake halisi lilikuwa Angela) kwa kisu tumboni na alipofikishwa hospitali madaktari waligundua alikuwa na uume wa bandia katika nguo zake.

Akisimulia mkasa huo, Eliza, alisema kamwe hajawahi kumwona Angelo akiwa uchi, na walikuwa wakifanya mapenzi gizani tu ambapo aliwahi kumwambia pia kwamba kuna mwanamke aliwahi kumchoma moto sehemu zake za siri kufuatia ugomvi uliotokea kati yao hapo zamani – jambo ambalo lilidhihirisha kwamba Angelo alikuwa anatumia kiungo hicho bandia wakati wakifanya mapenzi.

Ugunduzi huo ulionyesha Angelo alikuwa pia akijifanya mwanamke na mwanamme ambapo aliwafanyia ukatili kila mara ‘wenza’ wake hao.  Hayo yalithibitishwa na watu wengi walioleta ushahidi kwamba mtu huyo aliwahi kuwa ‘mume’ au mke wao.

Pamoja na kumuua Angelo, mashitaka dhidi ya Eliza, yalitupiliwa mbali baada ya kuonekana alikuwa anajihami dhidi ya mashambulizi ya ‘mumewe’ huyo.
       CHANZO: DAILY MAIL

Post a Comment

أحدث أقدم