CHADEMA yatangaza kiama cha CCM


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) itaondolewa madarakani na watumishi wa umma. Chama hicho kikuu cha upinzani kimesema kuwa, CCM itaondolewa madarakani iwapo haitapandisha mshahara wa kundi hilo kabla ya mwaka 2015.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi Chadema, John Mnyika, alisema nguzo pekee iliyobaki kwa CCM ni watumishi wa umma, ambao wanauwezo mkubwa wa kuiangusha.

Mnyika alisema ndani ya miaka miwili Chadema imefanikiwa kueneza sera na malengo yao na kufanikiwa kuungwa mkono kwa asilimia 90 ya Watanzania wasio watumishi wa umma.

Alisema kazi iliyobaki hivi sasa ni kukata nguzo hiyo iliyosalia ambayo ni watumishi wa umma na kuwataka walimu, madaktari na watumishi wengine wa idara zote za Serikali kuondoa hofu ya kupoteza ajira zao na kuungana na Chadema ili kuiondoa madarakani.

“Hatuingii Ikulu mwaka 2015 kwa fadhila wala hila za CCM, bali tunaingia kwa nguvu ya umma na ishara za nguvu ya umma zimejidhihirisha jinsi wananchi walivyounga mkono Vuguvugu la Mabadiliko (M4C).

“CCM itarajie nguvu kubwa mwaka unaoanza kesho (leo), baada ya ratiba ya kikao cha Kamati Kuu kukaa na kuweka mpango kazi, CCM isidhani inaweza kuisambaratisha Chadema kirahisi kama inavyofikiri.

“Kwanza wao wenyewe wameanza kutofautiana kauli, juzi Naibu Katibu Mkuu Bara, Mwigulu Nchemba amesema ifikapo 2016 Chadema itakuwa imekufa.

“Wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira aliwahi kusema Chadema itakufa baada ya mwaka mmoja sasa hapo nani mkweli?

“Ni vema CCM ikaachana na propaganda za uchaguzi wa mwaka 2015 na badala yake iwatumikie wananchi kwa kupanua vyanzo vya mapato na kutumia rasilimali za nchi ili watumishi wa umma waweze kuongezewa mshahara wao vinginevyo watajutia.

“Hadi sasa asilimia 90 ya wananchi wasio na kazi wanaunga mkono M4C na mara zote wamekuwa wakiwalaumu watumishi wa umma kwa kuiunga mkono CCM kwa kuhofia kibarua chao. Sasa tunawaomba kuungana nasi ili kuiondoa CCM madarakani,” alisema.

Mnyika alisema ameshangazwa na kitendo cha Nchemba kushindwa kutangaza majina ya wabunge

Post a Comment

أحدث أقدم