EDWARD LOWASA,KUZINDUA TOVUTI YA WANAHABARI MORO


 Mwenikiti wa chma cha waandishi mkoa wa Morogoro,Boniventure Mtalimbo[Kati] akisisitiza jambo kwenye mkutano wake na waandishi wa habari leo mchana,kuli ni mratibu wa shughuri hiyo Latiga Ganzel na kushoto ni maratibu wa [MORO PC] Thadei Hajigwa
                     Baadhi ya wana habari wakimsikiliza mwenyekiti huyo leo mchana
 Mwandishi mwandamizi wa gazeti la mwananchini Hamida Sharrif[mwenye gauni la kitenge] akimsikiliza kwa umakini mwenyekiti huyo
 

 Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa [kuli] akiteta jambo na waziri mkuu Mizengo Pinda[kati]kushoto ni mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Morogoro,lnjinia Petro Kingu na aliyekluwa jirani na mawaziri hao ni mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera
MBUNGE wa Monduli ambaye pia ni waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa anatarajiwa kuongoza shughuli za uzindizi wa mfuko  wa jamii pamoja na Tovuti ya chama cha waandishi wa habari mkoa wa Morogoro (MOROPC) wakati wa sherehe ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha 2013.


Hayo yalibainishwa  leo mchana na Mwenyekiti wa Muda wa Moropc Boniventure Mtalimbo wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye ofisi za chama hicho, na kusema uzinduzi huo utafanyika Januari 19 mwaka huu katika hoteli ya kitalii ya   Nashera mjini Morogoro.

Mtalimbo alisema  lengo la kuanzishwa kwa mfuko wa jamii ni kuwawezesha waandishi wahabari, kwenda vijijini kwaajili ya kuandika habari kutokana na maeneo hayo kushindwa kufikika kwa urahisi kutokana na ukosefu wafedha.

Aliongeza kusema kwamba mbali na waandishi kwenda vijijini pia utakuwa ukisaidia kwa mambo mbalimbali ikiwemo kwenye maafa, kama vile vifo, magonjwa pamoja na kuwawezesha kujiendeleza kielimu.

Akizungumzi uzinduzi wa tovuti (Website) alisema waandishi wa habari mkoani Morogoro watakuwa wakiandika makala mbalimbali zikiwemo za kuelimisha jamii,na kuandaa vipindi vya televisheni na redio na kuingiza kwenye tovuti hiyo.

 Pia Mwenyekiti huyo aliwaomba wadau mbalimbali ndani nanje ya mkoa wa Morogoro, kujitokeza kuchangiakwa hali na mali mfuko huo ili kuwawezesha waandishi hao kufanya kazi kwa ufanisi zaidi pamoja na kuibua mambo mbalimbali yaliyojificha hususani vijijini.

Aliwataja wadhamini waliojitokeza hadi sasa kuwa ni Hoteli ya Nashera, Banki ya CRDB, Mamlaka ya mapato Tanzania TRA,Kampuni ya Umeme ya Mac Dolnad Live line,Kampuni ya Abood, Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini  Azizi Abood, Mamlaka ya Maji safi na Taka mkoa wa Morogoro MORUWASA.
na dustan

Post a Comment

Previous Post Next Post