MALIKIA WA MIPASHO YAMFIKA



KWA siku mbili mfululizo, jana na juzi, ujumbe kupitia njia ya simu ulikuwa ukisambaa kwa kasi na kuvumisha kuwa mwimbaji gwiji wa miondoko ya taarab hapa nchini, Bi Khadija Kopa, amefariki dunia.
Juzi usiku Saluti5 ilimpigia simu Khadija Kopa baada ya uvumi huo kuzagaa, simu yake ikapokelewa na mtu mwingine na kusema kuwa kwa muda ule Bi Khadija tayari alikuwa ameshalala lakini mtu huyo akaithibitishia Saluti5 kuwa habari hizo si za kweli.
Jana jioni uvumi huo ukaibuka tena ambapo Saluti5 ilipokea simu nyingi za wasomaji wake zilizotaka kujua ukweli juu ya jambo hilo.
Saluti5 ilipoongea na Khadija Kopa jana usiku, alisema hajui uvumi huo umetokea wapi. “Labda kuna Khadija mwingine aliyefariki kwenye familia nyingine ya Kopa”, alisema Bi Khadija na kuongeza kuwa pengine pia ni njia ya watu kumtakia maisha marefu.
Chanzo:- Saluti5

Post a Comment

أحدث أقدم