Mama mmoja Kaskazini mwa India katika jimbo la Rajasthan, amekamatwa kwa madai ya kumuuza mwanawe kwa dola 12,000.
Mama huyo alisema kuwa alimuuza bintiye ili
aweze kupata pesa za kulipia faini aliyokuwa ametozwa ya dola elfu tano
na baraza la kijiji.Umaskini na hali ngumu ya maisha huwapelekea wanawake nchini India kuwauza watoto wao, na wasichama wengi pia huuzwa.
Polisi wanasema kuwa msichana huyo aliuzwa mwezi mmoja uliopita lakini uhalifu huo ulijulikana wakati alipojaribu kuwatoroka watu waliokuwa wanamnunua mtoto huyo.
Washukiwa walimfukuza lakini wakafanikiwa kuingia katika mkahawa mmoja ambapo watu walimtambua na kuita polisi.
Msichana huyo alimbia polisi kuwa watu waliokuwa wamemnunua walimchapa na walikuwa wanapanga kumuuza kwa watu wengine mjini Mumbai.
"tulimkamata mamake msichana huyu, na wanunuzi wawili,'' alinukuliwa akisema mkuu wa kitengo cha kupambana na uuzaji haramu wa watu.
Lakini baadaye alifutilia mbali makubaliano yake na mwanamume yule na kumchukua msichana wake. Na hapo ndipo baraza la wzee wa kijiji lilimtoza faini kwa kosa hilo.
Post a Comment