MIAKA 20 JELA KWA KOSA LA MAUAJI YA MWIGIZAJI

JUU: Gemma McCluskie. CHINI: Muuaji Tony Mc Cluskie. KULIA: Visu vilivyotumika kutekelezea mauaji hayo.
Kaka 'katili' wa mwigizaji wa Eastender Gemma McCluskie amehukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua na kutupa mwili alioukatakata vipande wa mwigizaji huyo kwenye mfereji.

Tony McCluskie alipatikana na hatia ya mauaji na jopo la mashitaka kwa watu 11 dhidi ya mmoja. Hapo awali alikiri kosa la kuua bila kukusudia.

Jana hakuonesha hisia zozote wakati alipohukumiwa kwenda jela maisha sambamba na kifungo cha miaka 20 jela kwenye gereza la Old Bailey.
Jaji huyo alisema Tony alifanya kila awezalo kuaibisha sifa ya dada yake huyo 'maarufu kwa kiasi kikubwa' wakati wa kesi hiyo.

Kulikuwa na kutweta na vilio kwenye chumba cha mahakama wakati hukumu, ambayo ilichukua chini ya siku mbili kufikia hapo, ilipokuwa ikisomwa lakini Tony alisimama bila hisia zozote kwenye kizimba chake.
Mwili uliokatwa viungo wa Gemma ulikutwa ukielea kwenye mfereji wa Regent huko mashariki mwa London, mahakama ya Old Bailey ilielezwa.

Tony, mwenye miaka 36 msafishaji madirisha na mvutaji mkubwa wa bangi, alidai alishindwa kujizuia baada ya matusi na kashfa nzito kutoka kwa dada yake.

Alisema kitu cha mwisho alichokumbuka ilikuwa ni dada yake kumfuata huku akiwa na kisu mkononi.
Lakini upande wa mashitaka ulisema alimuua dada yake huyo mwenye miaka 29 baada ya Gemma kushindwa kumvumilia Tony na kumtaka kuhama kwenye ghorofa hilo lililoko Shoreditch, mashariki mwa London, ambako walikuwa wakiishi.

Tukio la mwisho lilikuwa pale Tony alipoacha bomba likitoa maji na sinki kujaa na kumwaga maji chumba kizima Machi, mwaka jana.

Aliuawa baada ya kupigwa kichwani zaidi ya mara moja na mwili wake ulikatwa katika vipande sita kwa kutumia shoka na kisu.

Post a Comment

Previous Post Next Post