SERIKALI YAPUNGUZA MAKATO UWANJA WA TAIFA

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Amos Makala (kulia) akizungumza na Waandishi wa Habari, ofisini kwake katikati ya Jiji leo, kuhusu kupunguza makato ya mapato ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kukubali kulipa kodi za mishahara wa makocha wa timu ya taifa. Kulia ni Katibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah. 



Katibu wa TFF, Angetile Osiah akisaini hati ya makubaliano kuhusu matumizi ya Uwanja wa Taifa na mgawanyo wa mapato.

Mkurugenzi wa Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Mama Juliana Yasoda, akisaini hati ya makubaliano kuhusu matumizi ya Uwanja wa Taifa na mgawanyo wa mapato.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kamati ya Ligi Kuu, Silas Mwakibinga akisaini hati ya makubaliano kuhusu matumizi ya Uwanja wa Taifa na mgawanyo wa mapato.

Post a Comment

Previous Post Next Post