Tigo yaja na ‘Tigo Time’ punguzo la saa 24.

Kampuni ya Simu ya Tigo imetambulisha huduma mpya kwa wateja ujulikanayo kama Tigo Time , ambayo inatoa punguzo kubwa sana la gharama ya kupiga simu saa 24/7 ikitegemeana na wakati, siku na eneo atakapo kuwa mteja husika.
Mbunifu wa Ofa za Tigo Bi. Jacqueline Nnunduma (Pichani) amesema Tigo inatambua kwamba wateja wake wanahitaji huduma bora na kwa gharama nafuu nah ii ni njia moja wapo ya kuhakikisha kuwa wateja wao wanapata huduma zenye ubora wa juu na vifurushi ambavyo vitawapatia unafuu wa bei kwa muda wote.
Kwa punguzo hili kubwa la bei lililopita kifani, hakuna shaka kuwa Tigo Time itakuwa huduma maarufu kama ilivyo huduma ya ‘Kwa Sekunde’ iliyoanzishwa miaka kadhaa iliyopita.

Post a Comment

أحدث أقدم