Elizabeth Chijuba(Nikita) Sasa niko Fiti kabisa

Mwandishi mahiri wa miswada (Script) na muigizaji mkongwe katika filamu Tzee Elizabeth Chijuba maarufu Nikita amesema kwa sasa yupo fiti kabisa baada ya kusumbuliwa na tumbo hali iliyopelekea kukimbizwa haraka na kulazwa hospitali.

Nikita amesema anajisikia vizuri na yupo tayari kuendelea na shughuli zake za filamu.
Nikita amesema anawashukuru wote waliokuwa nae bega kwa bega katika kipindi chote cha ugonjwa wake na kutoa wito kwa wasanii kusaidiana na kupeana moyo kila mmoja anapopatwa na shida.

Post a Comment

Previous Post Next Post