Kamati Kuu Chama Cha Mapinduzi taifa (CCM) kujulikana Jumanne, Feb. 12,2013 huku Mwenyekiti Taifa (CCM), Rais Jakaya Kikwete akiwataka Wajumbe kupendekeza suluhisho la Ajira nchini.



Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akielekeza jambo wakati wa ufunguzi wa Semina maalum kwaajili ya wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM taifa iliyofanyika mjini Dodoma katika ukumbi wa White House makao makuu Februari 10,2013.


 
Kushoto anayesikiliza kwa makini ni Makamu  Mwenyekiti Mstaafu wa CCM bara Pius Msekwa.Wengine katika picha ni Rais Wa Zanzibar ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein(Wapili kushoto),Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdurahman Kinana(wanne kushoto), na kulia ni Makamu Mwenyekiti CCm Bara Ndugu Philip Mangula
Baadhi ya wajumbe wa kamati kuu ya CCM taifa wakihudhuria semina maalum iliyofunguliwa na kuongozwa na Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete katika ukumbi wa White House,Makao makuu ya CCM mjini Dodoma.



Aidha Mwenyekiti  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete akifungua  semina ya siku mbili ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM mjini Dodoma jana Februari 10,2013, ameponda makada wa chama hicho ambao wamekuwa wakipanda jukwaani kuhubiri kuwa ajira ni tatizo pasipo kupendekeza suluhisho la tatizo hilo.

 

Rais Kikwete alisema kusimama jukwaani na kusema kwamba ajira ni tatizo hakuna maana ikiwa mhusika hatoi pendekezo la jinsi ya kumaliza tatizo hilo.


Suala la ajira nchini ni moja ya mada zinazotarajiwa kuwasilishwa kisha kujadiliwa katika semina hiyo ya CCM, na Rais Kikwete aliwataka wajumbe kupendekeza jinsi ya kuongeza ajira nchini wakati mjadala husika utakapowadia.



Hata hivyo, Rais Kikwete alisema hivi sasa ajira katika sekta ya umma ni kama hakuna, kwani zimebaki sekta za afya na elimu na kwamba hivi sasa suluhu ni kukuza sekta binafsi ili kuongeza ajira.



Kamati  Kuu ya Chama Cha Mapinduzi taifa (CCM) itajulikana Jumanne, Feb. 12, mwaka huu, kisha kufanya kazi ya kuteua Kamati ya Maadili ya chama hicho.

Kupatikana kwa wajumbe hao kutatokana na kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) ambayo itakutana Feb. 11 mwaka huu, chini ya Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete na kufanya uchaguzi huo.

Post a Comment

Previous Post Next Post