Masheikh wa Somalia waapa kupambana na itikadi kali baada ya mtumishi kuuawa akiwa anasali

Viongozi kutoka Baraza la Kiislamu la al-Itisaam wakizungumza na waandishi wa habari katika Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki huko Garowe tarehe 19 Februari. Viongozi walisema kuwa watawatumia wanazuoni wa Somalia na wananchi kusimama pamoja dhidi ya vurugu na itikadi kali. [Hassan Muse Hussein/Sabahi]

Na Hassan Muse Hussein, Garowe na Barkhad Dahir, Hargeisa

Viongozi wa Somalia na wananchi walielezea kushtushwa kwao na kulaani baada ya kijana mmoja kumpiga risasi Sheikh Abdulkadir Nur Farah ndani ya Msikiti wa Badar huko Garowe wakati wa sala ya Asr Ijumaa iliyopita (tarehe 15 Februari).

Farah alipigwa risasi mgongoni wakati alipokuwa akiinama kusali.

Masaa baadaye, Rais wa Jimbo la Puntland Abdirahman Mohamed Farole aliwalaumu hadharani al-Shabaab kwa mauaji hayo ya sheikh maarufu wa Somalia, na kutangaza kukamatwa kwa Abdirahman Hussein Jama Bile kuhusiana na mauaji.

Siku ya Jumamosi, polisi wa Somaliland waliwatia mbaroni washukiwa wawili zaidi huko Las Anod kuhusika na mauaji hayo.

"Mmoja wa watu wawili hao ambaye yuko mikononi mwetu anaaminika kuhusika moja kwa moja na mauaji ya wiki iliyopita ya marehemu Sheikh Abdulkadir Nur Farah, wakati mshiriki mwenzake aliwezesha kutoroka kwake," Abdullahi Said Guleid, naibu kamanda wa polisi huko Sool, aliliambia gazeti la Dawan.

Alisema kuwa washukiwa walikamatwa wakati walikuwa wakiendesha gari kuelekea mjini, kiasi cha kilomita 150 magharibi ya Garowe. Watu hao wamehamishiwa Hargeisa na wako chini ya uchunguzi, Guleid alisema.

Suluhisho kwa itikadi kali

Sheikh Abdulkadir Nur Farah alizikwa katika makaburi ya kaskazini ya Garowe siku ya Jumamosi (tarehe 16 Februari). [Hassan Muse Hussein/Sabahi]

Viongozi wa kidini Somalia nzima walilaani mauaji hayo na kutoa wito kwa wananchi kutafuta suluhisho la siasa kali. "Tunalaani mauaji haya," alisema Sheikh Mubarak Haji Nur wa Buro, Somaliland. "Ni kinyume na misingi ya Uislamu na utamaduni [wa Somalia]."

Nur pia alitoa wito kwa viongozi wa dini na wa Somalia kusimama pamoja dhidi ya wale wanaomwaga damu za wasio na hatia.

Sheikh Ahmed Abdisamad, mtumishi wa huko Puntland na kiongozi wa kamati ya utendaji ya Balaza la al-Itisaam, kikundi cha kidini ambacho kiliapa kupambana na uenezaji wa itikadi ya al-Shabaab, alitangaza Jumanne (tarehe 19 Februari) kwamba yeye na viongozi wa dini nyingine wanapanga kufanya mkutano mkuu katika siku zijazo kufanya utafiti kwa ajili ya kuelewa vizuri chanzo ambacho kilisababisha wenye msimamo mkali nchini Somalia na kutoa suluhisho linalozingatia dini ambalo litatumika na umma.

Farole na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Somalia Mohamed Mohamud Guled walisema wanayakaribisha na watatoa msaada wao kamili kwa mkutano wa masheikh.

Abdisamad pia alipongeza mamlaka za Somaliland kwa kuwakamata washukiwa kwa haraka. Alihimiza tawala za eneo nchini Somalia kuwashirikisha wananchi ili kukabiliana kwa uthabiti dhidi ya al-Shabaab.

Ili kupambana na wenye msimamo mkali na kutafuta suluhisho thabiti, jamii za Somalia zinapaswa kushirikiana kushughulikia masuala yote yanayowakabili, alisema. Wakati kutokubaliana na matatizo yanapotokea, watu wanapaswa kurejea katika uongozi ulioundwa wa kitaaluma na kisiasa.

"Makabila yetu, watumishi, majimbo, wafanyabiashara, wanajeshi na vitengo vyote vya umma lazima viungane kwa lengo moja," aliiambia Sabahi.

Sheikh Abdinasir Haji Ahmed wa Las Anod pia alilaani al-Shabaab kwa mauaji hayo. "Sheikh huyo aliuawa na watu wakatili ndani ya al-Shabaab, hususan wanakikundi cha Amniyad ambacho kinasifika kama watu waliotengwa ambao wanawaua Waislamu."

Farah azikwa
Farah alizikwa katika makaburi ya kaskazini ya Garowe Jumamosi, mazishi yaliyohudhuriwa na watumishi wa dini kutoka Somalia nzima, wananchi na wawakilishi kutoka serikali ya Somalia na utawala wa Puntland.

Kabla ya kifo chake, Farah alieleza jinsi alivyoipinga al-Shabaab kwa nguvu zote, na alikuwa ni mwanachama wa Baraza la al-Itisaam.

"Wanajiita vijana wa jihadi, lakini jihadi yao inawalenga Waislamu," Farah alisema katika mawaidha katika Msikiti wa al-Rawda tarehe 5 Januari. "Wamewaua Waislamu wengi, na wote mnajua kwamba mamia ya Waislamu wanakufa katika milipuko. Ni wangapi walikufa kule Bosaso, Garowe na Galkayo wakati wakiingia au kutoka msikitini? … Hii ni aina yao ya jihadi."

Farah pia alizungumza katika mazishi ya Sheikh Ahmed Abdirahman, ambaye aliuawa mwezi Disemba 2011 huko Bosaso alipokua akiondoka kutoka Msikiti wa Al-Rawda baada ya sala ya alfajiri. Farah aliilaumu al-Shabaab kwa kifo cha Abdirahman.

Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni Wa Kiislamu siku ya Jumapili waliomboleza kifo cha Farah na walilaani mauaji yake.

"Jumuiya inatoa wito kwa watu wa Somalia kuungana dhidi ya itikadi kali ili kuwalinda watu wa jamii na kulinda maisha ya wanazuoni na raia wenye uwezo mkubwa," shirka hilo lilisema katika taarifa iliyotiwa saini na Mwenyekiti Yusuf al-Qaradawi na Katibu Mkuu Ali al-Qaradaghi.

Dahir Hassan,mwenye umri wa miaka 25 ambaye ni mwanafunzi wa masomo ya Kiislamu katika Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki huko Bosaso alisema hii ni mara yake ya kwanza kusikia mtu kuuwawa wakati anaswali. "Ilikuwa inatushangaza kujua kwamba mtu aliuawa baada ya kuondoka msikitini," aliiambia Sabahi.

Hassan alisema alitazama video katika mtandao wa Youtube ikionyesha kukamatwa kwa Bile na kumwita "kijana, mdogo mpotofu".

"Watu wanaouawa ni watumishi wetu wa dini, chanzo chetu cha maarifa," alisema Hassan, akiongeza kwamba utawala wa Puntland utapaswa kutoa walinzi wenye silaha kwa watumishi wa dini. "[Al-Shabaab] inataka kuondoa nguvu ya taifa hili na wanazuoni wake, hali ambayo itasababisha nchi yetu kukosa viongozi wasomi siku zijazo."

Post a Comment

أحدث أقدم