Mshindi wa Droo kubwa ya promosheni ya SmartCard ya Tigo apatikana

Menejawa Ubunifu  wa  ofa za Tigo David Sekwao (katikati) akizungumza na mshindi wa droo ya promosheni ya Tigo Smart Card kupitia simu ya kiganjani jijini Dar leo. Anayeshuhudia tukio hilo Kulia ni Ofisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Taifa ya kusimamia michezo ya kubahatisha.
Tigo Tanzania leo imetangaza mshindi wa droo kubwa ya promosheni ya smartcard  kuwa ni Bwana Julius Raphael Kanza ambaye ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam.
Bwana Kanza ameshinda zawadi kuu ambayo ni tiketi ya bure ya kwenda na kurudi Madrid Uhispania pamoja na kulipiwa gharama zote za safari kwenda kutizama  mechi  ya soka kati ya Real Madrid na FC Barcelona.
Alivyojulishwa kuhusu ushindi wake Bwana Kanza alifurahishwa sana na kusema “sikutegemea kabisa kuwa mshindi wa droo hii, nimefurahi sana na ninajiona wa muhimu sana. Napenda kuwashukuru Tigo kwa zawadi hii na nina hamu sana siku ziwadie niende kushuhudia mechi hii kubwa kati ya Real Madrid na FC Barcelona”.
“Droo hii ni mwendelezo wa droo za promosheni ya smartcard ambazo zinaendelea kufanyika  kila mwezi, robo mwaka, na kila mwaka. Promosheni ya smartcard ilizinduliwa Septemba 2012 hususan kwa ajili ya wateja wa Tigo ambao wanatumia smartphones kama Blackberry, Android na iphone.” Alisema Bwana David Sekwao meneja wa ubunifu wa ofa za Tigo.
Bwana Sekwao aliendelea kwa kusema kuwa “Mbali na zawadi kuu ya droo hii, washindi 42  watabahatika  kujishindia zawadi mbalimbali zikiwemo tiketi 12 za sinema, tiketi 12 za klabu, tiketi 12 za kuangalia mechi za mpira kwenye klabu ya hapa nchini, vocha 3 za kununua bidhaa mbalimbali na vocha 3 za chakula cha jioni.” Aliongeza kuwa “mshindi wa leo bwana Kanza atapatiwa tiketi ya bure ya kwenda na kurudi Madrid Uhispania na kulipiwa gharama zote za safari kwenda kuangalia mechi  ya soka kati ya Real Madrid na FC Barcelona ambazo ndio timu kuu za ligi ya Hispania La Liga”
Kushiriki katika shindano hili, mteja alitakiwa awe amejiunga na kifurushi cha Smartcard chenye thamani ya Tshs 30,000 kwa mwezi na awe ametumia huduma hii kwa miezi mitatu mfululizo na vilevile awe amejiunga na jamii ya smartcard kupitia www.tigo.co.tz/smartcardcommunity
Zawadi nyingine kuu za mwaka za droo hii ni pamoja na  tiketi ya ndege ya kwenda na kurudi Dubai, malazi ya siku 5 pamoja na hela ya matumizi kiasi cha shilingi laki moja na nusu kwa siku na vilevile tiketi na gharama za kwenda na kurudi Uingereza kuangalia mechi kati ya Arsenal na man United mwezi Aprili mwaka 2013.

Post a Comment

Previous Post Next Post