Msanii Linah Sanga siku alipokua Boston, Massachusetts nchini Marekani
Msanii wa kizazi kipya Linah Sanga amekanusha habari zilizotoka kwenye
mitandao ya kijamii kwamba anatoka kimapenzi na KIJANA aliyejipatia
umaarufu kwa 'kumvamia' msukuma kabumbu wa Real Madrid, ‘Kaka’ Nagari
Kombo.
Linah amekanusha vikali kuhusu habari hiyo
na kukemea mitandao inayoandika habari za mtu bila ya kuhakikisha
kwanza, aliendelea kwa kusema maisha ya mahusiano ni 'Private Life' ya
msanii, na kama kuna ulazima wa kuwekwa hadharani basi msubiri msanii
mwenyewe aongee, hata kama umesikia kitu na huna uhakika nacho, kwanini
usimuulize muhusika kusudi upate kusikia upande wa pili wa stori
unasemaje.
Msanii huyo wa kizazi kipya amelaani vikali habari hiyo na kuongezea
Nagari Kombo ni rafiki yake na sio kwamba ndiye anayemmiliki kimapenzi,
mimi ni SINGLE naomba muelewe hivyo na kama kuna lolote si msubiri
muambiwe jamani?
Post a Comment