Rais
  Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
 Bole jijini Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 23, 2013 kuhudhuria 
utiwaji saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na 
Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).(PICHA NA 
IKULU).
Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete 
amewasili Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 23, 2013 kuhudhuria 
utiwaji saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na 
Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Mpango
 huo unatarajiwa kutiwa saini kesho Februari 24, 2013 na Wakuu wa Nchi 
kutoka Ukanda wa Maziwa Makuu, ikiwa ni pamoja na Jamhuri ya 
Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Jamhuri ya Uganda, Jamhuri ya Afrika ya 
Kati, Jamhuri ya Angola, Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Kongo 
(Brazaville), Jamhuri ya Zambia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja 
na Jamhuri ya Afrika Kusini.
Aidha,
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe. Ban Ki Moon, Mwenyekiti wa 
Kamisheni ya Umoja wa Mataifa, Dkt. Nkosazana Dlamini-Zuma, pamoja na 
wenyeviti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Ukanda 
wa Maziwa Makuu (ICGLR) watatia saini Mpango huo kama mashahidi na 
wadhamini.
Mpango
 huo una nia ya kuchangia juhudi ambazo zimefanywa na Ukanda wa Maziwa 
Makuu (ICGLR) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) katika
 kutafuta amani Mashariki ya Kongo na ukanda wote wa Maziwa Makuu kwa 
ujumla.
Mpango
 huo pia umetilia maanani mapendekezo muhimu yaliyokubalika baada ya 
mashauriano kati ya wakuu wa nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) na 
Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Katibu Mkuu wa Umoja
 wa Mataifa.
Imetolewa na:
Muhidin Issa Michuzi,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
23 Februari, 2013


Post a Comment