TANZIA - DAR YOUNG AFRICAN


Uongozi wa klabu ya Yanga unasikitika kutangaza kifo cha mfanyakazi Hamza Said almaarufu kama Zola au Chiluba, kifo kilichotokea leo alfajiri kwa ajali ya kugongwa na gari katika makutano ya mitaa ya Rufiji/Congo.

Marehemu Zola alikua mfanyakazi katika Sekretatriet wa klabu ya Yanga mpaka unamkuta umauti alfajiri ya leo.

Taratibu za mazishi zitatolewa baadae baada ya uongozi kukaa na ndugu wa marehemu.

Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen
— at Young Africans Sports Club - HQ.

Post a Comment

أحدث أقدم