Umoja wa Mataifa UNAMID yataka waasi waache machafuko Sudan


Vikosi vya Kulinda Amani vya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa UNAMID huko Darfur Sudan vimeyataka makundi ya waasi kusitisha machafuko na vitendo vya utumiaji mabavu. 

Taarifa ya UNAMID imezitaka pande zote zinazozona katika jimbo la Darfur hususan makundi yanayobeba silaha na ambayo hayajajiunga na hati ya makubaliano ya amani kusitisha vitendo vya hujuma na kuheshimu sheria za kimataifa. 

Taarifa ya Vikosi vya Kulinda Amani vya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa UNAMID huko Darfur Sudan imesisitiza juu ya himaya ya Umoja wa Afrika, Umoja wa Mataifa na jamii ya kimataifa kwa hati ya makubaliano ya amani ya Darfur iliyotiwa saini katika mji mkuu wa Qatar, Doha. 

Hayo yanajiri katika hali ambayo, mwanzoni mwa mwezi huu wa Mei zaidi ya watu 130 waliuawa baada ya kutokea mapigano ya kikabila katika jimbo la Darfur magharibi mwa Sudan.

Post a Comment

أحدث أقدم