AFISA HABARI WA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA AJERUHIWA NA MAJAMBAZI NYUMBANI KWAKE

 Nkomola akiwa wodini amelazwa hii leo.
Nkomola akiwa na Mchumba wake Elizabeth wakati alipohudhuria send off yake huko Same.
  • Wamuibia fedha na vitu mbalimbali vya maandalizi ya harusi yake
  • wapora pia samani za ndani

Afisa Habari II Wizara ya Viwanda na Biashara,Edward Denis Nkomola  amevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo, nyumbani kwake Changanyikeni Dar es Salaam na kumjeruhi vibaya mwili.

Nkomola ni bwana harusi mtarajiwa na maandalizi ya harusi yake yapo katika hatua za mwisho ambao ndoa yake inataraji kufungwa Juni 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyo tolewa na Afisa Habari mwenzake wa Wizara hiyo, Thom Mushi kupitia mtandao wa facebook, inaelezwa kuwa tukio hilo lilimkuta Nkomola majira ya aa saba usiku, ambapo majambazi wanane wakiwa na silaha mbalimbali, walivamia nyumbani kwake na wakitaka wapewe fedha alizokusanya kwa ajili ya harusi yake.

Taarifa hiyo inasema kuwa kabla ya majambazi hao kufanikisha adhma yao hiyo walivunja mlango wa chuma (grill) na mlango wa kawaida wakimshambulia kwa mapanga na kumjeruhi kichwani kichwani, kumvunja  mkono, kumjeruhi kwa panga pajani na kumwibia samani za ndani, fedha na vifaa mbali mbali vya harusi.

Wiki iliyopita alitoka Wilayani Same kwenye Send Off ya mke wake Elizabeth.

Nkomola amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili katika kitengo cha Mifupa MOI akipatiwa matibabu na hali yake inaendelea kusimamiwa na madaktari kwa ukaribu zaidi.

Post a Comment

Previous Post Next Post