RIWAYA: ROHO MKONONI 5

Photo: RIWAYA: ROHO MKONONI
MTUNZI: George Iron Mosenya

SEHEMU YA TANO

Akafikiria ni wapi pengine anaweza kupata pesa, hakupata jibu. Na hapakuwa na njia yoyote ya kufanya haya bila pesa. Kwani ukiweka ada pembeni, yalihitajika madaftari, vitabu na sare za shule. Mara akamfikiria Dulla, hapa hakuumiza kichwa chake, kijana yule asingeweza kumsaidia kwa lolote.
Hatimaye akapitiwa na usingizi mzito bila kuwa na jibu sahihi. Cha ajabu asubuhi aliamka akiamini kuwa usiku alipata jibu. Na hili jibu alitakiwa kulifanyia kazi ili aone kama inawezekana kumpa furaha Joy.
“Aunt naenda kwa Joy…” aliaga baada ya kuwa amemaliza kazi zote za ndani.
“Mh haya na huyo Joy wako sijui siku akihama itakuwaje…mnavyopendana mwee!” shangazi yake Betty alimwambia huku akitabasamu. Maneno yale yakampa hulka zaidi Betty. Kumbe jamii inatambua kuwa wanapendana!!! Hadi shangazi yake……..
Betty akatoweka.

****

ZOEZI la ufuaji lilikuwa linaendelea huku redio ikiwa inapiga kelele ndani bila mtu yeyote kufanya jitihada za kuizimisha, licha ya redio kupiga na mfuaji mwenyewe alikuwa anapiga mluzi usioendana na wimbo wowote ule.
Mara mfuaji akahisi kuguswa sikio la kushoto akageukia upande wa kushoto, hola! Hakuna mtu. Akageukia upande wa kulia akakutana na muujiza. Muujiza wa aina yake.
“Shkamoo mwalimu!” alisalimiwa na kiumbe yule ambaye alionekana kama muujiza mbele yake.
“Marahaba…we mtoto wewe…hee karibu…karibu mpaka ndani.” Akakaribishwa huku yule mfuaji akiishia pale pale katika zoezi lake la ufuaji.
Wakaongozana na kuingia katika chumba kile kimoja kilichotenganishwa na pazia katikati na kufanya mfano wa vyumba viwili. Mgeni akaketi katika kiti cha mbao kilichokuwa katika kona ya nyumba. Akaangaza huku na kule katika nyumba ile, mara akaona hereni, akaguna kidogo.
“Ehe utatumia soda gani mrembo wewe.”
“Hapana sitatumia chochote kile. Ninahitaji kukaa kidogo tu kisha niondoke.” Alijibu. Mwenyeji akalazimisha hatimaye akaomba aletewe Fanta.
Baada ya muda walikuwa katika maongezi mazito na soda ikiwa mezani, bila kunyweka.
“Kwa hiyo ni hivyo nina shida sana na sijaona msaada mwingine zaidi ya kuja kwako, walau unaweza kunishauri ama kunisaidia kama unaweza.” Alimalizia yule msichana.
“Umesema unataka elfu hamsini…..lakini kwa nini umenifuata mimi eeh.”
“Kwa sababu naamini kama unaweza kunisaidia utanisaidia.” Alijibu kwa ufupi.
“Vipi kwanza Dula mzima.” Aliuliza lile swali kinafiki.
“Yupo tu anakusalimia.” Binti naye alijibu kinafiki. Kwani alijua kuwa yule mwalimu alikuwa akimchukia sana Dula kutokana na kijana yule kumpumbaza kimapenzi Betty, wakati na yeye alikuwa akimuhitaji sana. Mada juu ya Dula ikazua ukimya wa sekunde kadhaa kisha mwalimu akatupia chambo, “Nitakusaidia lakini iwapo nawe utanisaidia Betty.”
“Una maana gani?” aliuliza huku kichwani akitambua yule mwalimu ana maanisha nini.
“Hali ya hewa leo Makambako baridi kali. Nilikuwa najiuliza sana nitaishi vipi leo kwani we husikii baridi?.” Swali hili lilimalizika Mwalimu akiwa mbele ya Betty.
Alipoona Betty hana amani, akafunua lile pazia akakiendea kitanda akabenjua godoro akapekua kidogo akatoka na noti kadhaa. Macho ya Betty yakaona pesa kisha hapo hapo akaona chupi mbili za kike, akaguna tena kidogo. Mara yule mwalimu akamkabidhi ile pesa.
“Mimi nimemaliza msaada wangu, bado wewe.”
“Ticha ila…ila ni kwa leo tu na Dulla asijue tafadhali mwalimu.” Betty alisihi, kwa maana hiyo alikuwa amempa nafasi mwalimu kufanya lolote lakini kwa siku hiyo moja tu.
Mwalimu yule ambaye hana ugeni kwa wasichana na mapenzi kwa ujumla. Alimvamia Betty na kumrusha kitandani.
Betty alikuwa akiogopa sana kile kilichokuwa kinaenda kutokea, lakini ilikuwa lazima akipokee.
Yote haya kwa sababu ya kutii ndoto yake juu ya kipi afanye kumsaidia rafiki yake kipenzi.

****
JOYCE alikuwa anapalilia shamba la nyanya lililokuwa mbali kidogo na nyumba yao, alikuwa na masaa matatu tangu alipoanza shughuli hiyo. Kwa mbali aliwaona watu wakiwa wanaonyeshea vidole mahali alipokuwa, mmoja alikuwa ni msichana ambaye walikuwa wanaishi naye hapo nyumbani na mwingine alikuwa mgeni machoni pake. Hakujishughulisha kuwatazama akaendelea na kilimo hadi pale alipomuona yule mtu aliyekuwa mgeni machoni akijongea pale shambani.
“Hee kumbe wewe Jesca, ulivyojitanda leo hata nikakusahau.” Joy alisema huku akitabasamu. Akaegemea mpini wa jembe lile huku akimtazama Jesca.
“Shkamoo da’ Joy.”
“Marahaba Jesca ehee wazima huko nyumbani.” Aliuliza
“Wazima tu nimeagizwa hii..” alionyeshea bahasha ndogo ya kaki. Joy akatoka pale shambani na kumsogelea Jesca.
“Nani kakuagiza?”
“Da Betty.” Alijibu huku akimkabidhi kisha akaaga na kutoweka.

Wakati Jesca anatoweka Joy alimuona kwa mbali mama mwenye mji akiwa anasogea kule shambani, upesi akaipachika ile bahasha katika nguo yake ya ndani kisha akaendelea na kilimo.


SAA TATU USIKU.

Joy akiwa amemaliza kuosha vyombo baada ya kuwa wamekula, tayari alikuwa ameoga. Sasa aliikumbuka ile bahasha ambayo kwa muda ule ilikuwa chini ya kitanda, akaifunua upesi upesi huku akijiuliza Betty kamwandikia nini maana haikuwa kawaida yao kutumiana barua.
Akauendea mlango wa chumba chake akaufunga vyema, akaifungua bahasha ile kwa uangalifu mkubwa huku akishindwa kubashiri ndani ya bahasha ile kuna kitu gani.
Alhamdulilah! Noti saba rangi ya bluu zikamwagika sakafuni, Joyce akatokwa na yowe dogo la hofu. Hakuwa amewahi kukutana na kiasi kikubwa cha pesa, noti za bluu, kwa malipo ya shilingi elfu kumi. Akazikamata vyema kabla hajakutana na karatasi jingine, hili lilikuwa limeandikwa maneno kadhaa.
Akazificha zile pesa kisha akaketi kitandani, akaisogeza taa ya kandili ikamulika vizuri naye akaweza kusoma vyema.


Dear, Joyce

Naamini hapo ulipo hauna furaha hata kidogo na hakuna chochote cha kukuletea furaha. Naamini hauna ndugu wa karibu hapa Makambako zaidi ya rafiki ambaye ni mimi Joy.
Sitaki kusema kuwa nalipa wema lakini ni heri iwe hivyo. Naikumbuka sura yako siku uliyojaribu kumtolea mama yangu damu. Ukaokoa maisha yake, ulipigwa kwa sababu yangu. Kamwe wema wako haufanani na chochote ninachoweza kujaribu kusema.
Ningefanya nini Joyce walau ufurahi kidogo rafiki yangu mpenzi, kamwe nisingeweza kufurahi tena iwapo ungetoweka duniani bila mimi kujaribu kukupigania.
Joy mpenzi wangu. Tatizo lako ni tatizo langu na limeniumiza kichwa sana. Unadhani ningefanya nini kama si kujaribu kukupigania. Ni kweli sina biashara na unajua kuwa nyumbani kwetu si matajiri na mbaya zaidi ninaishi kwa ndugu tu.
Neno hili nakwambia wewe kwa maandishi haya kwa sababu sitaweza kusema kwa maneno na wala sitamweleza mtu yeyote tena. Nakwambia haya wewe ukiwa shahidi yangu kuwa sijawahi kuwa na mwanaume mwingine zaidi ya Dulla, nipo wazi kwako kwa kila kitu kama ndugu yangu wa dhati. Na unajua kuwa nampenda Dull asana. Lakini leo nakuandikia neno hili kuwa Dulla hana nafasi linapotokea tatizo linalokukabili wewe Joyce….” Joyce akachukua kanga yake akajifuta machozi, machozi ya furaha, nenohili kutoka kwa rafiki yake lilikuwa limemgusa sana.
Kisha akaendelea….

“Kama wewe ulivyompigania mama yangu na kuwanyima baba na mama yako nafasi basi name nipo hivyo.
Naamini kuwa kuna kitu niliwahi kukwambia, kuwa mwalimu Japhari alikuwa akinisumbua na alikuwa anamchukia Dulla. Mimi na wewe tukaungana kumchukia pia.
Lakini niseme tena hili, adui yeyote awezaye kumsaidia mwanadamu ninayempenda basi adui huyo huwa rafiki kwa muda. Joy ni wewe ninayekupenda, basi niliamua Japhari awe rafiki yangu, rafiki wa muda ilimradi tu wewe ambaye ni wa muhimu upate furaha walau kidogo. Hakika yule adui amenisaidia….amenipa hizo pesa.” Joyce akakoma kidogo kisha akajisemea “Jamani Betty, Mungu sijui umpe nini rafiki huyu….”
Akarejesha macho yake katika barua.
“Lakini alinipa kwa masharti, Joy yalikuwa masharti magumu, lakini kwa mema yote uliyowahi kunitendea sharti pekee ambalo linaweza kunishinda iwapo natakiwa kukusaidia ni kwenda kwa mganga tu nadhani unakumbuka kuwa nilikwambia siamini mambo hayo.
Joy mpenzi, Mwalimu alinitaka kimapenzi. Nilijaribu kujitetea lakini nikajikuta katika maamuzi mawili tu, niondoke bila pesa wewe Joyce ukose furaha, ama niondoke na pesa baada ya kumpa penzi.
Wewe ni rafiki na zaidi ya ndugu kwangu, sijisikii vibaya kukwambia kuwa Dulla akigundua yeye aniache tu Mungu atakuwa hajapanga lakini nafsi yangu ina furaha sana. Hiyo pesa Joy mbona shule tunaenda wote. Ifiche sana wala usishawishike kuitumia hata kidogo. Wewe acha tukazane tusome mpenzi si unajua huku Makambako sio kwetu tuna mtihani mkubwa sana wa kukikwamua kisiwa chetu cha Ukala.
Nina ombi moja kwako. Sihitaji tgukikutana uniulize jambo lolote juu ya kilichotokea.
Uwe na amani Joy.
Akupendaye kwa dhati, Betty.

Joyce alikuwa analia kwa kwikwi. Kuna ladha ya upendo ilikuwa inawakilishwa na machozi yale. Alijizuia asilie kwa sauti kubwa, akafanikiwa. Akaikunja ile barua, akaihifadhi mahali ambapo ni yeye tu angeweza kuijua.

****

KWELI, ilibaki kama walivyokubaliana. Mara moja!! Mara moja kweli!! Mwalimu Japhari alijaribu kwa kila namna kumshawishi Betty waweze kushiriki tena tendo lakini haikuwezekana, Betty alilichukulia jambo lile kana kwamba halikuwahi kutokea katika maisha yake. Joyce naye akaendelea kudumu na ile siri aliyoitunza kwa muda mrefu.
Suala la ndoa likasahaulika baada ya Joyce kufanikiwa kuwashawishi walezi wake kuwa amepata mtu wa kumlipia ada, hivyo atasoma hadi kifato cha nne ndipo ataolewa na huyo bwana, ukatokea mvutano lakini hatimaye mshindi akawa Joyce.
Muda ukafika Joyce na Betty wakaanza maisha mapywa katika shule ya upili Makambako. Ilikuwa furaha ya aina yake kwa wawili hawa kuwa pamoja tena.
Maisha yakaendelea katika namna ya kutia moyo hadi ilipofika tarehe 19 mwezi wa tatu mwaka 2002. Siku isiyosahaulika kamwe katika vichwa vya watu wengi lakini iliwaumiza zaidi Betty na Joyce.

ILIKUWA taarifa mbaya sana, Joyce alijiuliza anaanza vipi kumweleza Betty lakini hata kama asingemweleza bado tu angeipata kwa namna yoyote ile.
Muda wa mapumziko, Joyce alimsaka Betty na kumvuta kando kisha kwa masikitiko makubwa na wasiwasi hadharani akamweleza jambo.
“Mwalimu Japhari amefariki.” Alisema kwa masikitiko makubwa.
“Wacha wee!! Amejifia bora kero zipungue maana alitaka kunigombanisha na Dulla yule” Betty alisema kwa shangwe kubwa. Joyce hakuungana naye…bali akaendelea kuongea. “amekufa kwa UKIMWI Betty…..”
Hapa sasa Betty akatulia kidogo akapepesa macho huku na kule. Kisha akamtazama Joyce.
Kwa mara ya kwanza tangu ampe onyo katika ile barua kuwa asimuulize chochote Joyce akavunbja masharti.
“Betty….mlitumia kinga….” Akamuuliza..
“Mhh Mhh” akakataa Betty huku akizidi kutingwa na hofu. Kisha akatia neno, “Hivi anaweza kuwa kaniambukiza na mimi eti!!” aliuliza swali la kipumbavu Betty. Joyce hakulijibu.
“Kesho twende tukapime Betty wangu.” Joyce akashauri, shauri likapita.

Siku ikaisha katika namna ya kipekee, Joyce na Betty wakiwa hawana furaha.
Siku iliyofuata ilihitimisha kiza kinene, kiza kisichofahamika hatma yake. Kiza cha kutisha sana.
Machozi hayakuwa tiba ya matokeo aliyotoa daktari. Betty alikuwa mwathirika wa ‘homa ya Makambako’, lile gonjwa hatari la Ukimwi lilikuwa limemkumba mwanafunzi huyu wa kidato cha pili.
‘CD4’ zake zilikuwa imara sana, hakutetereka kwa muda wote tangu afanye mapenzi na Marehemu mwalimu Japhary.
Lakini mwezi wa sita mwaka huo huo 2002, ile siri haikuwa siri tena. Betty akajikuta yu katika kuugua ‘Ukimwi wa kishamba’ ule Ukimwi wa kuhara, kutapika na mkanda wa jeshi wa ajabu.
Ilisikitisha kumtazama, ikiwa tu ulikuwa umemwona miezi kadhaa nyuma.

Kila mtu alitambua kuwa siku za Betty zilikuwa zinahesabika. Hata Joyce alikiri kuwa rafiki yake kipenzi angekufa muda wowote.
Kila siku alimtembelea nyumbani kwao alipokuwa anauguzwa. Siku ambayo hakumkuta Betty katika kitanda kile.
Yakajirudia yaleyale ya Ukala. Betty alitoweka na hakuna hata mmoja aliyejua wapi amekwenda. Wapo waliosema kuwa Betty alikuwa marehemu tayari na wapo waliodai ameenda kutupwa katika mapori ya Malawi afie huko.
Hakuna aliyekuwa na jibu sahihi, hata Joyce alibaki katika sintofahamu na nyumbani kwao hawakutaka kuulizwa lolote juu ya wapi alipo Betty.
Maisha ya upweke yakarejea tena!! Shule nzima ikazizima. Yule mtaalamu wa somo la Kiswahili na hesabu katika shule yao alikuwa ametoweka. Kila mmoja alilalamika na kuweka hisia alizozifahamu yeye.
Wengi walidhani kuwa Joyce anafahamu lolote kuhusu Betty lakini hakuna alilofahamu zaidi ya kutambua kuwa marehemu mwalimu Japhari ndiye aliyemuambukiza.

**HISTORIA imebadilika….BETTY ametoweka hakuna ajuaye wapi alipo…….nini kinajiri…yawezekana amekufa kweli???

***JOYCE anashikiria siri nzito sana…..na hana mpango wa kuitoa kwa mtu yeyote yule.

**ROHO MKONONI imefikia panapoleta jina hili…..USIKOSE SEHEMU IJAYO..
COMMENTS zako ni za msingi sana ili kuwekana sawa…..

ITAENDELEA…..

RIWAYA: ROHO MKONONI


MTUNZI: George Iron Mosenya

SEHEMU YA TANO

Akafikiria ni wapi pengine anaweza kupata pesa, hakupata jibu. Na hapakuwa na njia yoyote ya kufanya haya bila pesa. Kwani ukiweka ada pembeni, yalihitajika madaftari, vitabu na sare za shule. Mara akamfikiria Dulla, hapa hakuumiza kichwa chake, kijana yule asingeweza kumsaidia kwa lolote.
Hatimaye akapitiwa na usingizi mzito bila kuwa na jibu sahihi. Cha ajabu asubuhi aliamka akiamini kuwa usiku alipata jibu. Na hili jibu alitakiwa kulifanyia kazi ili aone kama inawezekana kumpa furaha Joy.
“Aunt naenda kwa Joy…” aliaga baada ya kuwa amemaliza kazi zote za ndani.
“Mh haya na huyo Joy wako sijui siku akihama itakuwaje…mnavyopendana mwee!” shangazi yake Betty alimwambia huku akitabasamu. Maneno yale yakampa hulka zaidi Betty. Kumbe jamii inatambua kuwa wanapendana!!! Hadi shangazi yake……..
Betty akatoweka.

****

ZOEZI la ufuaji lilikuwa linaendelea huku redio ikiwa inapiga kelele ndani bila mtu yeyote kufanya jitihada za kuizimisha, licha ya redio kupiga na mfuaji mwenyewe alikuwa anapiga mluzi usioendana na wimbo wowote ule.
Mara mfuaji akahisi kuguswa sikio la kushoto akageukia upande wa kushoto, hola! Hakuna mtu. Akageukia upande wa kulia akakutana na muujiza. Muujiza wa aina yake.
“Shkamoo mwalimu!” alisalimiwa na kiumbe yule ambaye alionekana kama muujiza mbele yake.
“Marahaba…we mtoto wewe…hee karibu…karibu mpaka ndani.” Akakaribishwa huku yule mfuaji akiishia pale pale katika zoezi lake la ufuaji.
Wakaongozana na kuingia katika chumba kile kimoja kilichotenganishwa na pazia katikati na kufanya mfano wa vyumba viwili. Mgeni akaketi katika kiti cha mbao kilichokuwa katika kona ya nyumba. Akaangaza huku na kule katika nyumba ile, mara akaona hereni, akaguna kidogo.
“Ehe utatumia soda gani mrembo wewe.”
“Hapana sitatumia chochote kile. Ninahitaji kukaa kidogo tu kisha niondoke.” Alijibu. Mwenyeji akalazimisha hatimaye akaomba aletewe Fanta.
Baada ya muda walikuwa katika maongezi mazito na soda ikiwa mezani, bila kunyweka.
“Kwa hiyo ni hivyo nina shida sana na sijaona msaada mwingine zaidi ya kuja kwako, walau unaweza kunishauri ama kunisaidia kama unaweza.” Alimalizia yule msichana.
“Umesema unataka elfu hamsini…..lakini kwa nini umenifuata mimi eeh.”
“Kwa sababu naamini kama unaweza kunisaidia utanisaidia.” Alijibu kwa ufupi.
“Vipi kwanza Dula mzima.” Aliuliza lile swali kinafiki.
“Yupo tu anakusalimia.” Binti naye alijibu kinafiki. Kwani alijua kuwa yule mwalimu alikuwa akimchukia sana Dula kutokana na kijana yule kumpumbaza kimapenzi Betty, wakati na yeye alikuwa akimuhitaji sana. Mada juu ya Dula ikazua ukimya wa sekunde kadhaa kisha mwalimu akatupia chambo, “Nitakusaidia lakini iwapo nawe utanisaidia Betty.”
“Una maana gani?” aliuliza huku kichwani akitambua yule mwalimu ana maanisha nini.
“Hali ya hewa leo Makambako baridi kali. Nilikuwa najiuliza sana nitaishi vipi leo kwani we husikii baridi?.” Swali hili lilimalizika Mwalimu akiwa mbele ya Betty.
Alipoona Betty hana amani, akafunua lile pazia akakiendea kitanda akabenjua godoro akapekua kidogo akatoka na noti kadhaa. Macho ya Betty yakaona pesa kisha hapo hapo akaona chupi mbili za kike, akaguna tena kidogo. Mara yule mwalimu akamkabidhi ile pesa.
“Mimi nimemaliza msaada wangu, bado wewe.”
“Ticha ila…ila ni kwa leo tu na Dulla asijue tafadhali mwalimu.” Betty alisihi, kwa maana hiyo alikuwa amempa nafasi mwalimu kufanya lolote lakini kwa siku hiyo moja tu.
Mwalimu yule ambaye hana ugeni kwa wasichana na mapenzi kwa ujumla. Alimvamia Betty na kumrusha kitandani.
Betty alikuwa akiogopa sana kile kilichokuwa kinaenda kutokea, lakini ilikuwa lazima akipokee.
Yote haya kwa sababu ya kutii ndoto yake juu ya kipi afanye kumsaidia rafiki yake kipenzi.

****
JOYCE alikuwa anapalilia shamba la nyanya lililokuwa mbali kidogo na nyumba yao, alikuwa na masaa matatu tangu alipoanza shughuli hiyo. Kwa mbali aliwaona watu wakiwa wanaonyeshea vidole mahali alipokuwa, mmoja alikuwa ni msichana ambaye walikuwa wanaishi naye hapo nyumbani na mwingine alikuwa mgeni machoni pake. Hakujishughulisha kuwatazama akaendelea na kilimo hadi pale alipomuona yule mtu aliyekuwa mgeni machoni akijongea pale shambani.
“Hee kumbe wewe Jesca, ulivyojitanda leo hata nikakusahau.” Joy alisema huku akitabasamu. Akaegemea mpini wa jembe lile huku akimtazama Jesca.
“Shkamoo da’ Joy.”
“Marahaba Jesca ehee wazima huko nyumbani.” Aliuliza
“Wazima tu nimeagizwa hii..” alionyeshea bahasha ndogo ya kaki. Joy akatoka pale shambani na kumsogelea Jesca.
“Nani kakuagiza?”
“Da Betty.” Alijibu huku akimkabidhi kisha akaaga na kutoweka.

Wakati Jesca anatoweka Joy alimuona kwa mbali mama mwenye mji akiwa anasogea kule shambani, upesi akaipachika ile bahasha katika nguo yake ya ndani kisha akaendelea na kilimo.


SAA TATU USIKU.

Joy akiwa amemaliza kuosha vyombo baada ya kuwa wamekula, tayari alikuwa ameoga. Sasa aliikumbuka ile bahasha ambayo kwa muda ule ilikuwa chini ya kitanda, akaifunua upesi upesi huku akijiuliza Betty kamwandikia nini maana haikuwa kawaida yao kutumiana barua.
Akauendea mlango wa chumba chake akaufunga vyema, akaifungua bahasha ile kwa uangalifu mkubwa huku akishindwa kubashiri ndani ya bahasha ile kuna kitu gani.
Alhamdulilah! Noti saba rangi ya bluu zikamwagika sakafuni, Joyce akatokwa na yowe dogo la hofu. Hakuwa amewahi kukutana na kiasi kikubwa cha pesa, noti za bluu, kwa malipo ya shilingi elfu kumi. Akazikamata vyema kabla hajakutana na karatasi jingine, hili lilikuwa limeandikwa maneno kadhaa.
Akazificha zile pesa kisha akaketi kitandani, akaisogeza taa ya kandili ikamulika vizuri naye akaweza kusoma vyema.


Dear, Joyce

Naamini hapo ulipo hauna furaha hata kidogo na hakuna chochote cha kukuletea furaha. Naamini hauna ndugu wa karibu hapa Makambako zaidi ya rafiki ambaye ni mimi Joy.
Sitaki kusema kuwa nalipa wema lakini ni heri iwe hivyo. Naikumbuka sura yako siku uliyojaribu kumtolea mama yangu damu. Ukaokoa maisha yake, ulipigwa kwa sababu yangu. Kamwe wema wako haufanani na chochote ninachoweza kujaribu kusema.
Ningefanya nini Joyce walau ufurahi kidogo rafiki yangu mpenzi, kamwe nisingeweza kufurahi tena iwapo ungetoweka duniani bila mimi kujaribu kukupigania.
Joy mpenzi wangu. Tatizo lako ni tatizo langu na limeniumiza kichwa sana. Unadhani ningefanya nini kama si kujaribu kukupigania. Ni kweli sina biashara na unajua kuwa nyumbani kwetu si matajiri na mbaya zaidi ninaishi kwa ndugu tu.
Neno hili nakwambia wewe kwa maandishi haya kwa sababu sitaweza kusema kwa maneno na wala sitamweleza mtu yeyote tena. Nakwambia haya wewe ukiwa shahidi yangu kuwa sijawahi kuwa na mwanaume mwingine zaidi ya Dulla, nipo wazi kwako kwa kila kitu kama ndugu yangu wa dhati. Na unajua kuwa nampenda Dull asana. Lakini leo nakuandikia neno hili kuwa Dulla hana nafasi linapotokea tatizo linalokukabili wewe Joyce….” Joyce akachukua kanga yake akajifuta machozi, machozi ya furaha, nenohili kutoka kwa rafiki yake lilikuwa limemgusa sana.
Kisha akaendelea….

“Kama wewe ulivyompigania mama yangu na kuwanyima baba na mama yako nafasi basi name nipo hivyo.
Naamini kuwa kuna kitu niliwahi kukwambia, kuwa mwalimu Japhari alikuwa akinisumbua na alikuwa anamchukia Dulla. Mimi na wewe tukaungana kumchukia pia.
Lakini niseme tena hili, adui yeyote awezaye kumsaidia mwanadamu ninayempenda basi adui huyo huwa rafiki kwa muda. Joy ni wewe ninayekupenda, basi niliamua Japhari awe rafiki yangu, rafiki wa muda ilimradi tu wewe ambaye ni wa muhimu upate furaha walau kidogo. Hakika yule adui amenisaidia….amenipa hizo pesa.” Joyce akakoma kidogo kisha akajisemea “Jamani Betty, Mungu sijui umpe nini rafiki huyu….”
Akarejesha macho yake katika barua.
“Lakini alinipa kwa masharti, Joy yalikuwa masharti magumu, lakini kwa mema yote uliyowahi kunitendea sharti pekee ambalo linaweza kunishinda iwapo natakiwa kukusaidia ni kwenda kwa mganga tu nadhani unakumbuka kuwa nilikwambia siamini mambo hayo.
Joy mpenzi, Mwalimu alinitaka kimapenzi. Nilijaribu kujitetea lakini nikajikuta katika maamuzi mawili tu, niondoke bila pesa wewe Joyce ukose furaha, ama niondoke na pesa baada ya kumpa penzi.
Wewe ni rafiki na zaidi ya ndugu kwangu, sijisikii vibaya kukwambia kuwa Dulla akigundua yeye aniache tu Mungu atakuwa hajapanga lakini nafsi yangu ina furaha sana. Hiyo pesa Joy mbona shule tunaenda wote. Ifiche sana wala usishawishike kuitumia hata kidogo. Wewe acha tukazane tusome mpenzi si unajua huku Makambako sio kwetu tuna mtihani mkubwa sana wa kukikwamua kisiwa chetu cha Ukala.
Nina ombi moja kwako. Sihitaji tgukikutana uniulize jambo lolote juu ya kilichotokea.
Uwe na amani Joy.
Akupendaye kwa dhati, Betty.

Joyce alikuwa analia kwa kwikwi. Kuna ladha ya upendo ilikuwa inawakilishwa na machozi yale. Alijizuia asilie kwa sauti kubwa, akafanikiwa. Akaikunja ile barua, akaihifadhi mahali ambapo ni yeye tu angeweza kuijua.

****

KWELI, ilibaki kama walivyokubaliana. Mara moja!! Mara moja kweli!! Mwalimu Japhari alijaribu kwa kila namna kumshawishi Betty waweze kushiriki tena tendo lakini haikuwezekana, Betty alilichukulia jambo lile kana kwamba halikuwahi kutokea katika maisha yake. Joyce naye akaendelea kudumu na ile siri aliyoitunza kwa muda mrefu.
Suala la ndoa likasahaulika baada ya Joyce kufanikiwa kuwashawishi walezi wake kuwa amepata mtu wa kumlipia ada, hivyo atasoma hadi kifato cha nne ndipo ataolewa na huyo bwana, ukatokea mvutano lakini hatimaye mshindi akawa Joyce.
Muda ukafika Joyce na Betty wakaanza maisha mapywa katika shule ya upili Makambako. Ilikuwa furaha ya aina yake kwa wawili hawa kuwa pamoja tena.
Maisha yakaendelea katika namna ya kutia moyo hadi ilipofika tarehe 19 mwezi wa tatu mwaka 2002. Siku isiyosahaulika kamwe katika vichwa vya watu wengi lakini iliwaumiza zaidi Betty na Joyce.

ILIKUWA taarifa mbaya sana, Joyce alijiuliza anaanza vipi kumweleza Betty lakini hata kama asingemweleza bado tu angeipata kwa namna yoyote ile.
Muda wa mapumziko, Joyce alimsaka Betty na kumvuta kando kisha kwa masikitiko makubwa na wasiwasi hadharani akamweleza jambo.
“Mwalimu Japhari amefariki.” Alisema kwa masikitiko makubwa.
“Wacha wee!! Amejifia bora kero zipungue maana alitaka kunigombanisha na Dulla yule” Betty alisema kwa shangwe kubwa. Joyce hakuungana naye…bali akaendelea kuongea. “amekufa kwa UKIMWI Betty…..”
Hapa sasa Betty akatulia kidogo akapepesa macho huku na kule. Kisha akamtazama Joyce.
Kwa mara ya kwanza tangu ampe onyo katika ile barua kuwa asimuulize chochote Joyce akavunbja masharti.
“Betty….mlitumia kinga….” Akamuuliza..
“Mhh Mhh” akakataa Betty huku akizidi kutingwa na hofu. Kisha akatia neno, “Hivi anaweza kuwa kaniambukiza na mimi eti!!” aliuliza swali la kipumbavu Betty. Joyce hakulijibu.
“Kesho twende tukapime Betty wangu.” Joyce akashauri, shauri likapita.

Siku ikaisha katika namna ya kipekee, Joyce na Betty wakiwa hawana furaha.
Siku iliyofuata ilihitimisha kiza kinene, kiza kisichofahamika hatma yake. Kiza cha kutisha sana.
Machozi hayakuwa tiba ya matokeo aliyotoa daktari. Betty alikuwa mwathirika wa ‘homa ya Makambako’, lile gonjwa hatari la Ukimwi lilikuwa limemkumba mwanafunzi huyu wa kidato cha pili.
‘CD4’ zake zilikuwa imara sana, hakutetereka kwa muda wote tangu afanye mapenzi na Marehemu mwalimu Japhary.
Lakini mwezi wa sita mwaka huo huo 2002, ile siri haikuwa siri tena. Betty akajikuta yu katika kuugua ‘Ukimwi wa kishamba’ ule Ukimwi wa kuhara, kutapika na mkanda wa jeshi wa ajabu.
Ilisikitisha kumtazama, ikiwa tu ulikuwa umemwona miezi kadhaa nyuma.

Kila mtu alitambua kuwa siku za Betty zilikuwa zinahesabika. Hata Joyce alikiri kuwa rafiki yake kipenzi angekufa muda wowote.
Kila siku alimtembelea nyumbani kwao alipokuwa anauguzwa. Siku ambayo hakumkuta Betty katika kitanda kile.
Yakajirudia yaleyale ya Ukala. Betty alitoweka na hakuna hata mmoja aliyejua wapi amekwenda. Wapo waliosema kuwa Betty alikuwa marehemu tayari na wapo waliodai ameenda kutupwa katika mapori ya Malawi afie huko.
Hakuna aliyekuwa na jibu sahihi, hata Joyce alibaki katika sintofahamu na nyumbani kwao hawakutaka kuulizwa lolote juu ya wapi alipo Betty.
Maisha ya upweke yakarejea tena!! Shule nzima ikazizima. Yule mtaalamu wa somo la Kiswahili na hesabu katika shule yao alikuwa ametoweka. Kila mmoja alilalamika na kuweka hisia alizozifahamu yeye.
Wengi walidhani kuwa Joyce anafahamu lolote kuhusu Betty lakini hakuna alilofahamu zaidi ya kutambua kuwa marehemu mwalimu Japhari ndiye aliyemuambukiza.

**HISTORIA imebadilika….BETTY ametoweka hakuna ajuaye wapi alipo…….nini kinajiri…yawezekana amekufa kweli???

***JOYCE anashikiria siri nzito sana…..na hana mpango wa kuitoa kwa mtu yeyote yule.

**ROHO MKONONI imefikia panapoleta jina hili…..USIKOSE SEHEMU IJAYO..
COMMENTS zako ni za msingi sana ili kuwekana sawa…..

ITAENDELEA…

Post a Comment

Previous Post Next Post