SIMULIZI: USILIE NADIA 6



Photo: SIMULIZI: USILIE NADIA
MTUNZI: George iron mosenya
SIMU: 0655 727325

SEHEMU YA SITA

“Waliosema wema hawagandi alikuwa na maana yake, wema huyeyuka upesi. Jadida ambaye alikuwa mwanga wangu naye akapotea katika namna ya ajabu, hivi yawezekana mimi nilikuwa na bahati kuwa walinifanya vile kisha wakaniacha hai. Jadida…aaah Jadida yaani wakakufanyisha mapenzi kinyume na maumbile kisha wakakuua, hivi uliwaamini kwa nini watu wale, kwanini uliwaamini Jadida. Kumbe Jadida nawe hukuwa nma ndugu, serikali ikakufukia kama mzoga tu…ni mkimi pekee niliyesikitika wengine walisema alikufa akifanya uchangudoa….Jadida ambona uliondoka mapema sasa eeh!!” hapa hakuweza tena kuongea, alikuwa ameuma meno yake kwa hasira sana. Na machozi yalikuwa yanamtiririka.
Upesi nikaita taksi, ikatupakia na kuturudisha hotelini.
Nikiwa natazama mbele nilikuwa nawaza na kuwazua. Mkasa huu ulikuwa mtata kweli, ulikuwa mkasa unaozua maswali mengi na majibu machache.
MOJA: NADIA alifanya uchangudoa kumbe DES alimtimua? Alitoa wapi ujasiri huo.
MBILI: Akalawitiwa akifanya uchangudoa….akaacha uchangudoa halafu??
TATU: JADIDA alimwongoza katika njia ipi sasa?
NNE: DES ana akili kweli yaani anamzushia mtu kuwa ana majini?? Vipi dua za Nadia zitamkumba Desmund??


*******
Tulipofika hotelini sikuhitaji Nadia aseme neno lolote la ziada maana hakika alikuwa amechoka, alikuwa Amelia haswa. Na alikuwa na hasira.
Mawazo aliyokuwa nayo hakika yalikuwa yakimtafuna ndani kwa ndani. Nilijisikia vibaya kama vile alikuwa dada yangu wa kuzaliwa tumbo moja.
Niliamini kuwa hata Nadia atakuwa amechoka na atakuwa anahitaji kupumzika lakini sikuwa sahihi hata kidogo.
Tulipofika chumbani Nadia aliendelea kuzungumza, sasa kwa hasira zaidi tofauti na wakati ule tulipokuwa nje.
“Japo nilihisi nimetengwa na kila kitu na dunia ikiwa imenitukana kila aina ya tusi, naweza kukiri kuwa Jadida alikuwa mwanamke ambaye alikuwa zaidi ya ndugu kwangu. Alinisimamia hadi dakika ya mwisho, hakika niliujua umuhimu wake kiukweli lakini niliutambua vyema baada ya kuhakikishiwa kuwa Jadida hatarudi tena alikuwa amekufa. Moja kwa moja!!
Nilibaki katika kile chumba alichokuwa akiishi na wale machangudoa wengine.
Baada ya majuma mawili nikaanza kuombwa pesa ya matumizi, ama la nitajua jinsi nitakavyokula mimi mwenyewe.
Mwandishi ujue tangu nilipoingiliwa kinyume na maumbile sikutaka kabisa kujiingiza katika katika uchangudoa. Hata Jadida alisema nisijiingize tena, yeye atajiuza name nitakula na kulala bila mashaka, sasa hayupo tena watu wabaya walikuwa wamemuua, ni hapa nilipoanza kujiona mkiwa tena na kisha kujiuliza hivi nilizaliwa kwa ajili ya kuteseka, nikamlilia Mungu na kuona kwa hakika sikutakiwa kuendelea kuadhibiwa baada ya yote niliyopitia. Hata kama ilikuwa adhabu basi ilikuwa imetosha. Lakini Mungu hapangiwi, nilibaki kunung’unika tu huku nikiendelea kuteseka. Baada ya kunivumilia siku kadhaa hatimaye likafuata suala la kulipa kodi ya pango, hapa sikuonewa huruma yoyote, nilitakiwa kuchangia pango.
Ningetoa wapi pesa na Jadi hakuwepo!! Nikaumiza akili yangu sana kisha nikamkumbuka Ramadhani ama Ramso…” akasita kidogo, kisha akanitazama kwa uchungu mkuu.
“Mwandishi yaani ni basi tu sina mtoto, ni basi tu nasema sikuweza kuzaa lakini kama ningekuwa na kizazi nisingeweza kumwita mtoto wangu jina hilo hata kidogo, yaani nisingeweza kumwita Rama nasema. Yaani basi tu hatukupewa uwezo wa kujua lijalo nasema jambo hili kwa mara nyingine lakini laiti tungewezeshwa kujua huenda ningeliepuka.
Na bado haya yote yalitokea kwa sababu tu Jadi hakuwepo maana Rama alikuwa amenitongoza siku nyingi sana lakini sikuwahi kumkubalia, naweza kukiri kuwa ule urembo wangu ulikuwa umeanza kuchepua tena baada ya matunzo mazuri kutoka kwa Jadida na ilikuwa lazima wanaume waanze kunitamani, kweli Rama akaanza kunitongoza mara kwa mara lakini Jadi aliyesimama kama dada yangu alinikemea kabisa, lakini sasa Jadida amekufa. Natakiwa kulipa kodi nikajikuta sina kimbilio zaidi ya Rama. Nikamtafuta mwenyewe na kumweleza kuwa nina shida na shilingi elfu tatu, alkanitazama kisha akakumbushia lile lengo lake la awali kuhusu kunitaka kimapenzi. Nilijua lazima tu atataka kitu hicho, nikajikuta katika maamuzi ya aina mbili tu nikose mahali pa kulala nikalale stendi wahuni wanibake bila kunipa hata senti tano ama nikubali kufanya mapenzi na Rama anipe hiyo pesa nikalipie pango niendelee kulala sehemu ambayo walau kidogo ina usalama.

Tukakubaliana na Rama kuwa nitaenda kuchukua nyumbani kwake, na sio nyumba bali ni chumba kikubwa. Majira ya saa tisa sitasahau ilikuwa saa tisa na robo maana saa kilikuwa kitu cha kwanza kuangalia baada ya kuingia katika chumba chake. Niliketi katika stuli iliyokuwa wazi, Rama akaniuliza natumia kinywaji gani nikaagiza maji, nililetewa nikayanywa huku nikijisikia aibu kuu, aibu kwa sababu nilikuwa pale kwa ajili ya kudhalilishwa. Nadia mimi niliyeitunza bikira yangu hadi chuo kikuu leo hii nauza ngono. Nauza nipate pesa ya kulipia chumba.
Niliumia sana kwa kweli, lakini wakati naumia katika nafsi Rama alikuwa akiniita majina ya kimahaba ambayo hayakuwa na maana kwangu, huwezi kuniita mpenzi mtu kama mimi ambaye nilijiona kama uchafu tu.
Alipotaka kunivutia kitandani nilimsihi kitu kimoja kuwa nilikuwa nina njaa kali, hakika sikuwa namdanganya yaani baada ya kuwa nimekula muhogo mmoja asubuhi hiyo sikuwa nimepata kitu chochote tena. Kweli Rama alitoka nje na kisha akaingia na sahani ya wali nikauvamia na kwa fujo, kisha nikashushia na maji. Sasa hapa niliweza kumridhisha Rama. Tukapanda kitandani anifanye anachotaka.
Akafanya kweli huku nikimzuga kuwa ninafurahia tendo lile. Lakini sikuwa pale hata kidogo.
Rama akamaliza, nikadhani nimemaliza kulipa deni lakini mara kutokea chini ya kitanda wakatokea wanaume wengine watatu ambao naweza kuwaita wababe.
Nikamuuliza Rama kulikoni akaanza kuniambia jambo ambalo sikutarajia hata kidogo mwanaume anaweza kufanya hivyo.
Rama akadai kuwa nilijifanya mjanja sana kumkatalia kimapenzi mapema, sasa nitamkoma yeye sio wa kuzungushwa hovyo. Nilijaribu kujitetea huku nikimtupia lawama dada Jadida lakini haikusaidia, wale wanaume wakaanza kuniingilia kwa zamu, nikiwa nimezibwa na kanga yangu mdomoni. Ramso ameketi akivuta sigara huku akicheka, mwandishi sio siri niliumia mno, nilijitahidi kuwahimili lakini walinizidi kwa nguvu, nikajikuta sasa nazizima!! Nikaanza kuona maluweluwe tupu!!
Na bado niliwasikia wanaendelea kuniingilia……
Kabla sijapoteza fahamu kuna mabo niliyasikia wakisemezana na sikujua yana maana gani maana ni kama nilikuwa nasikia kiarabu na kihindi ikiwa lugha wanayotumia. Masikio yalisikia kama kengere kali sana zikipigwa. Kisha kimya kikatanda…..kimya kikuu.
Nilikuja kushtuka usiku sana nikiwa kando kando ya maji ya ziwa viktoria. Nilijaribu kusimama lakini nilianguka tena, nikajaribu kupiga kelele lakini sauti haikuweza kutoka, nikaanza kujikongoja huku nikiwa nimepatwa na hali fulani iliyonikumbusha jambo fulani, nilijaribu kupingana na hali hiyo lakini ukweli ulikuwa huu huu ninaokueleza sasa. Rama akishirikiana na washirika wake walikuwa wamenifanyisha mapenzi kinyume na maumbile. Nilizidi kutambaa gizani, mara mbwa wakaanza kubweka. Walibweka hasa kisha wakanifikia nilipokuwa, mbwa mmoja akanisukuma chini na kuanza kunikwangua na makucha yake. Nilijaribu kujitetea lakini haikuwezekana, mara akaongezeka mbwa mwingine huyu alinivamia moja kwa moja na kuning’ata mkono wangu hapa (akajifunua mkono na kunionyesha kovu). Nililia kwa nguvu mara akafika mmiliki wa hizo mbwa, huyu alikuwa ni mlinzi. Akawafukuza wale mbwa. Akanimulika na tochi huku akiniuliza mimi ni nani, wakati huo sikuwa na nguo mwili, mbwa walizigawana.
Labda hata hili lilikuwa tatizo lililonifanya nizidi kuuchukia usiku ule mgumu kupindukia.
Yule mlinzi kijana alizima tochi yangu, akanisogelea na kujifanya anataka kunisaidia, lakini na yeye akanifanya vibaya. Alinibaka upesiupesi kisha akajiondokea, nilidhani ameondoka kweli lakini haikuwa hivyo alikuwa ameenda kuwashirikisha na walinzi wengine wenye tamaa.
Wawili wakanikuta nikiwa bado pale, mmoja aliomba sana niachwe kama nilivyo lakini bahati mbaya hakuwa mbabe kuliko wenzake. Mwenye nguvu akashinda nikabakwa tena. Kwa mara nyingine nikapoteza fahamu.
Nilikuja kushtuka alfajiri, bado sikuwa na nguo. Lakini kabla sijajua nini cha kufanya mara akina mama wanaowahi katika biashara zao asubuhi walinikuta nikiwa pale bila hili wala lile. Wakanipa msaada wa kanga wakiamini mimi ni changudoa niliyepata ajali kazini.
Labda walikuwa sawa….lakini siamini kama nilizaliwa kuwa changudoa.
Fadhaa ile ikanifanya nijikute katika maamuzi ya aina yake, maamuzi ya kurejea Musoma kudai changu….ni lazima nipewe changu…..ama la! Desmund anieleze kwanini aliamua kunitenda vile.
Sikuwa na la kupoteza kwa sasa, nikajikuta napoteza rasmi tabasamu langu, bila shaka roho ya Jadida ilinivamia…..niaamua kurejea Musoma kulisaka jibu la matatizo hayo. Maana haiwezekani yaani nimelawitiwa kisa Desmund, nikabakwa tena na teana kisa yeye, halafu anaendelea kuyafurahia maisha wakati mimi nadhalilishwa hapana Hapana mwandishi, mnyonge mnyongeni lakini haki yake……” Nadia hakuweza kumalizia, akaingia katika kilio cha kwikwi.
“Usilie nadia, nipo kwa ajili yako kama nilivyokwambia sawa!!” nilimweleza kwa sauti ya chini. Kisha nikamvuta na kumkumbatia. Hapa sasa akaanza kulia kwa sauti ya juu kabisa.
Kwa sababu hakuwa akiniona, nami uvumilivu ukanishinda nikajikuta natokwa na chozi hadharani kwa mara ya kwanza tangu nianze kuifuatilia simulizi hii ya Nadia.


***HAYA Nadia uvumilivu umemshinda….ameamua kurejea MUSOMA kwao Desmund…nini kitrajiri…
##USIKOSE KESHO SIMULIZI HII YA NADIA….atatusimulia nini kiliendelea…JE MNYONGE ALIIPATA HAKI YAKE……
****TOA MAONI YAKO****
SIMULIZI: USILIE NADIA


MTUNZI: George iron mosenya

SIMU: 0655 727325

SEHEMU YA SITA


“Waliosema wema hawagandi alikuwa na maana yake, wema huyeyuka upesi. Jadida ambaye alikuwa mwanga wangu naye akapotea katika namna ya ajabu, hivi yawezekana mimi nilikuwa na bahati kuwa walinifanya vile kisha wakaniacha hai. Jadida…aaah Jadida yaani wakakufanyisha mapenzi kinyume na maumbile kisha wakakuua, hivi uliwaamini kwa nini watu wale, kwanini uliwaamini Jadida. Kumbe Jadida nawe hukuwa nma ndugu, serikali ikakufukia kama mzoga tu…ni mkimi pekee niliyesikitika wengine walisema alikufa akifanya uchangudoa….Jadida ambona uliondoka mapema sasa eeh!!” hapa hakuweza tena kuongea, alikuwa ameuma meno yake kwa hasira sana. Na machozi yalikuwa yanamtiririka.
Upesi nikaita taksi, ikatupakia na kuturudisha hotelini.
Nikiwa natazama mbele nilikuwa nawaza na kuwazua. Mkasa huu ulikuwa mtata kweli, ulikuwa mkasa unaozua maswali mengi na majibu machache.
MOJA: NADIA alifanya uchangudoa kumbe DES alimtimua? Alitoa wapi ujasiri huo.
MBILI: Akalawitiwa akifanya uchangudoa….akaacha uchangudoa halafu??
TATU: JADIDA alimwongoza katika njia ipi sasa?
NNE: DES ana akili kweli yaani anamzushia mtu kuwa ana majini?? Vipi dua za Nadia zitamkumba Desmund??


*******
Tulipofika hotelini sikuhitaji Nadia aseme neno lolote la ziada maana hakika alikuwa amechoka, alikuwa Amelia haswa. Na alikuwa na hasira.
Mawazo aliyokuwa nayo hakika yalikuwa yakimtafuna ndani kwa ndani. Nilijisikia vibaya kama vile alikuwa dada yangu wa kuzaliwa tumbo moja.
Niliamini kuwa hata Nadia atakuwa amechoka na atakuwa anahitaji kupumzika lakini sikuwa sahihi hata kidogo.
Tulipofika chumbani Nadia aliendelea kuzungumza, sasa kwa hasira zaidi tofauti na wakati ule tulipokuwa nje.
“Japo nilihisi nimetengwa na kila kitu na dunia ikiwa imenitukana kila aina ya tusi, naweza kukiri kuwa Jadida alikuwa mwanamke ambaye alikuwa zaidi ya ndugu kwangu. Alinisimamia hadi dakika ya mwisho, hakika niliujua umuhimu wake kiukweli lakini niliutambua vyema baada ya kuhakikishiwa kuwa Jadida hatarudi tena alikuwa amekufa. Moja kwa moja!!
Nilibaki katika kile chumba alichokuwa akiishi na wale machangudoa wengine.
Baada ya majuma mawili nikaanza kuombwa pesa ya matumizi, ama la nitajua jinsi nitakavyokula mimi mwenyewe.
Mwandishi ujue tangu nilipoingiliwa kinyume na maumbile sikutaka kabisa kujiingiza katika katika uchangudoa. Hata Jadida alisema nisijiingize tena, yeye atajiuza name nitakula na kulala bila mashaka, sasa hayupo tena watu wabaya walikuwa wamemuua, ni hapa nilipoanza kujiona mkiwa tena na kisha kujiuliza hivi nilizaliwa kwa ajili ya kuteseka, nikamlilia Mungu na kuona kwa hakika sikutakiwa kuendelea kuadhibiwa baada ya yote niliyopitia. Hata kama ilikuwa adhabu basi ilikuwa imetosha. Lakini Mungu hapangiwi, nilibaki kunung’unika tu huku nikiendelea kuteseka. Baada ya kunivumilia siku kadhaa hatimaye likafuata suala la kulipa kodi ya pango, hapa sikuonewa huruma yoyote, nilitakiwa kuchangia pango.
Ningetoa wapi pesa na Jadi hakuwepo!! Nikaumiza akili yangu sana kisha nikamkumbuka Ramadhani ama Ramso…” akasita kidogo, kisha akanitazama kwa uchungu mkuu.
“Mwandishi yaani ni basi tu sina mtoto, ni basi tu nasema sikuweza kuzaa lakini kama ningekuwa na kizazi nisingeweza kumwita mtoto wangu jina hilo hata kidogo, yaani nisingeweza kumwita Rama nasema. Yaani basi tu hatukupewa uwezo wa kujua lijalo nasema jambo hili kwa mara nyingine lakini laiti tungewezeshwa kujua huenda ningeliepuka.
Na bado haya yote yalitokea kwa sababu tu Jadi hakuwepo maana Rama alikuwa amenitongoza siku nyingi sana lakini sikuwahi kumkubalia, naweza kukiri kuwa ule urembo wangu ulikuwa umeanza kuchepua tena baada ya matunzo mazuri kutoka kwa Jadida na ilikuwa lazima wanaume waanze kunitamani, kweli Rama akaanza kunitongoza mara kwa mara lakini Jadi aliyesimama kama dada yangu alinikemea kabisa, lakini sasa Jadida amekufa. Natakiwa kulipa kodi nikajikuta sina kimbilio zaidi ya Rama. Nikamtafuta mwenyewe na kumweleza kuwa nina shida na shilingi elfu tatu, alkanitazama kisha akakumbushia lile lengo lake la awali kuhusu kunitaka kimapenzi. Nilijua lazima tu atataka kitu hicho, nikajikuta katika maamuzi ya aina mbili tu nikose mahali pa kulala nikalale stendi wahuni wanibake bila kunipa hata senti tano ama nikubali kufanya mapenzi na Rama anipe hiyo pesa nikalipie pango niendelee kulala sehemu ambayo walau kidogo ina usalama.

Tukakubaliana na Rama kuwa nitaenda kuchukua nyumbani kwake, na sio nyumba bali ni chumba kikubwa. Majira ya saa tisa sitasahau ilikuwa saa tisa na robo maana saa kilikuwa kitu cha kwanza kuangalia baada ya kuingia katika chumba chake. Niliketi katika stuli iliyokuwa wazi, Rama akaniuliza natumia kinywaji gani nikaagiza maji, nililetewa nikayanywa huku nikijisikia aibu kuu, aibu kwa sababu nilikuwa pale kwa ajili ya kudhalilishwa. Nadia mimi niliyeitunza bikira yangu hadi chuo kikuu leo hii nauza ngono. Nauza nipate pesa ya kulipia chumba.
Niliumia sana kwa kweli, lakini wakati naumia katika nafsi Rama alikuwa akiniita majina ya kimahaba ambayo hayakuwa na maana kwangu, huwezi kuniita mpenzi mtu kama mimi ambaye nilijiona kama uchafu tu.
Alipotaka kunivutia kitandani nilimsihi kitu kimoja kuwa nilikuwa nina njaa kali, hakika sikuwa namdanganya yaani baada ya kuwa nimekula muhogo mmoja asubuhi hiyo sikuwa nimepata kitu chochote tena. Kweli Rama alitoka nje na kisha akaingia na sahani ya wali nikauvamia na kwa fujo, kisha nikashushia na maji. Sasa hapa niliweza kumridhisha Rama. Tukapanda kitandani anifanye anachotaka.
Akafanya kweli huku nikimzuga kuwa ninafurahia tendo lile. Lakini sikuwa pale hata kidogo.
Rama akamaliza, nikadhani nimemaliza kulipa deni lakini mara kutokea chini ya kitanda wakatokea wanaume wengine watatu ambao naweza kuwaita wababe.
Nikamuuliza Rama kulikoni akaanza kuniambia jambo ambalo sikutarajia hata kidogo mwanaume anaweza kufanya hivyo.
Rama akadai kuwa nilijifanya mjanja sana kumkatalia kimapenzi mapema, sasa nitamkoma yeye sio wa kuzungushwa hovyo. Nilijaribu kujitetea huku nikimtupia lawama dada Jadida lakini haikusaidia, wale wanaume wakaanza kuniingilia kwa zamu, nikiwa nimezibwa na kanga yangu mdomoni. Ramso ameketi akivuta sigara huku akicheka, mwandishi sio siri niliumia mno, nilijitahidi kuwahimili lakini walinizidi kwa nguvu, nikajikuta sasa nazizima!! Nikaanza kuona maluweluwe tupu!!
Na bado niliwasikia wanaendelea kuniingilia……
Kabla sijapoteza fahamu kuna mabo niliyasikia wakisemezana na sikujua yana maana gani maana ni kama nilikuwa nasikia kiarabu na kihindi ikiwa lugha wanayotumia. Masikio yalisikia kama kengere kali sana zikipigwa. Kisha kimya kikatanda…..kimya kikuu.
Nilikuja kushtuka usiku sana nikiwa kando kando ya maji ya ziwa viktoria. Nilijaribu kusimama lakini nilianguka tena, nikajaribu kupiga kelele lakini sauti haikuweza kutoka, nikaanza kujikongoja huku nikiwa nimepatwa na hali fulani iliyonikumbusha jambo fulani, nilijaribu kupingana na hali hiyo lakini ukweli ulikuwa huu huu ninaokueleza sasa. Rama akishirikiana na washirika wake walikuwa wamenifanyisha mapenzi kinyume na maumbile. Nilizidi kutambaa gizani, mara mbwa wakaanza kubweka. Walibweka hasa kisha wakanifikia nilipokuwa, mbwa mmoja akanisukuma chini na kuanza kunikwangua na makucha yake. Nilijaribu kujitetea lakini haikuwezekana, mara akaongezeka mbwa mwingine huyu alinivamia moja kwa moja na kuning’ata mkono wangu hapa (akajifunua mkono na kunionyesha kovu). Nililia kwa nguvu mara akafika mmiliki wa hizo mbwa, huyu alikuwa ni mlinzi. Akawafukuza wale mbwa. Akanimulika na tochi huku akiniuliza mimi ni nani, wakati huo sikuwa na nguo mwili, mbwa walizigawana.
Labda hata hili lilikuwa tatizo lililonifanya nizidi kuuchukia usiku ule mgumu kupindukia.
Yule mlinzi kijana alizima tochi yangu, akanisogelea na kujifanya anataka kunisaidia, lakini na yeye akanifanya vibaya. Alinibaka upesiupesi kisha akajiondokea, nilidhani ameondoka kweli lakini haikuwa hivyo alikuwa ameenda kuwashirikisha na walinzi wengine wenye tamaa.
Wawili wakanikuta nikiwa bado pale, mmoja aliomba sana niachwe kama nilivyo lakini bahati mbaya hakuwa mbabe kuliko wenzake. Mwenye nguvu akashinda nikabakwa tena. Kwa mara nyingine nikapoteza fahamu.
Nilikuja kushtuka alfajiri, bado sikuwa na nguo. Lakini kabla sijajua nini cha kufanya mara akina mama wanaowahi katika biashara zao asubuhi walinikuta nikiwa pale bila hili wala lile. Wakanipa msaada wa kanga wakiamini mimi ni changudoa niliyepata ajali kazini.
Labda walikuwa sawa….lakini siamini kama nilizaliwa kuwa changudoa.
Fadhaa ile ikanifanya nijikute katika maamuzi ya aina yake, maamuzi ya kurejea Musoma kudai changu….ni lazima nipewe changu…..ama la! Desmund anieleze kwanini aliamua kunitenda vile.
Sikuwa na la kupoteza kwa sasa, nikajikuta napoteza rasmi tabasamu langu, bila shaka roho ya Jadida ilinivamia…..niaamua kurejea Musoma kulisaka jibu la matatizo hayo. Maana haiwezekani yaani nimelawitiwa kisa Desmund, nikabakwa tena na teana kisa yeye, halafu anaendelea kuyafurahia maisha wakati mimi nadhalilishwa hapana Hapana mwandishi, mnyonge mnyongeni lakini haki yake……” Nadia hakuweza kumalizia, akaingia katika kilio cha kwikwi.
“Usilie nadia, nipo kwa ajili yako kama nilivyokwambia sawa!!” nilimweleza kwa sauti ya chini. Kisha nikamvuta na kumkumbatia. Hapa sasa akaanza kulia kwa sauti ya juu kabisa.
Kwa sababu hakuwa akiniona, nami uvumilivu ukanishinda nikajikuta natokwa na chozi hadharani kwa mara ya kwanza tangu nianze kuifuatilia simulizi hii ya Nadia.


***HAYA Nadia uvumilivu umemshinda….ameamua kurejea MUSOMA kwao Desmund…nini kitrajiri…
##USIKOSE KESHO SIMULIZI HII YA NADIA….atatusimulia nini kiliendelea…JE MNYONGE ALIIPATA HAKI YAKE……
****TOA MAONI YAKO***

Post a Comment

Previous Post Next Post