Hata watanzania wanaweza ila basi tuu


Mwang'oka akiwa ndani ya gari lake

Umeuona mlango? Mwang'oka akishuka garini
Akifunga mlango

Akionyesha siti ya abiria wake

Juu tumeweka kupitisha upepo


Umeona dashboard yake ilivyo

Mbunifu Kenneth Joseph Mwang'oka akiwa katika pozi

Gari hilo linaloonekana kwa mbele

Kishoka napiga hivi

Bomba la kutolea moshi ndilo hili

Watu wakilishangaa gaari hilo

Umeona vitendea kazi vyake

Usukani wake ni mbao tu kweli msimu ni mali

Muonekano wa gari hilo kwa nyuma

rivasi kama kawa

TANZANIA imejaliwa watu wenye vipaji na ujuzi mkubwa katika nyanja ya Sayansi na Teknolojia ila kuna vitu vidogo vinavyowakwaza kusimama na kwenda sambamba na wataalam wa mataifa mengine ambao wapo mbali katika suala la vipaji na ubunifu.
Mifano michache ni watu wanaomudu kutengeneza magobole, mashine mbalimbali na vitu vingine na hata wabunifu wa mrusho wa matangazoi ya radio, ambao badala ya kuwezeshwa hupata vikwazo ikiwamo kunaswa na vyombo vya dola na kufunguliwa mashtaka ilihali wangeweza kutumika kuitangaza Tanzania.
Hapo juu ni mmoja wa wabunifu wa Kitanzania aliyeweza kutengeneza gari ambalo alitumia muda wa miezi sita kulikamilisha kwa kuokoteza vifaa na kulipambana kiasilia kwa kutumia malighafi ya misitu.
Majina yake kamili ni Kenneth Joseph Mwang'oka ambaye alikuwa moja ya vivutio katika Maonyesho ya Biashara ya Sabasaba kwa ubunifu wa gari hilo linalotumia injini ya Toyota na kuongeza ubunifu wao kiasi kwamba gari hilo lililomgharimu kiasi cha Sh Milioni 8.6 kutembea kutoka sehemu mbalimbali nchini.
Mwenyeji huyo wa mkoa wa Mbeya, lakini ubunifu wake kaufanyia mjini Iringa anasema lengo lake ni kuhakikisha anakuja kuntengeneza vitu zaidi ya gari hilo la aina yake.

Post a Comment

Previous Post Next Post