Msichana aliyewahi kuolewa na sasa anajiuza mwili asimulia biashara hiyo ilivyo - Fema Radio Show


Kipindi cha wiki hii cha Fema Radio Show kimezungumzia biashara ya mapenzi iliyoshamiri maeneo ya mjini.Katika kipindi hicho, mmoja wa wasichana wanaofanya kazi hiyo, Aisha amesimulia jinsi alivyoingia kwenye biashara hiyo baada ya kuvunjika kwa ndoa yake.
“Nilikuwa nimeolewa, niligombana na mume wangu, matatizo tu ya ndani ya ndoa, kwahiyo nikawa nimerudi nyumbani, pakawa na matatizo, tena matatizo ya kifamilia, maisha magumu, ndio ikabidi niingie kwenye kazi hiyo unayoiona,” anasema Aisha.
Aisha anasema mwanzoni alikuwa anajisikia vibaya kufanya kazi hiyo lakini kwa sasa ameshazoea.
“Mimi bado mgeni sijazoeleka, kuna wenyeji wapo wana miaka saba kwahiyo wanakuwa wameshazoeleka, mtu akipita wanajua wanamuitaje mpaka mtu anawakubalia kwahiyo inakuwa sio rahisi kwa wewe kupata mtu wa kwenda naye au kukupa hela.”
“Nachojutia mimi ni kukosa kazi ya kueleweka. Nimejifunza cherehani, sijaipenda tu kazi ya kushona, sina hobby na ufundi cherehani.”

Post a Comment

Previous Post Next Post