Ndege ya shirika la Asiana yapata ajali ilipokuwa ikitua uwanja wa ndege wa San Francisco na kuuwa wawili

Ndege ya shirika la Asiana,iliyokuwa ikitoka Seoul, kusini mwa Korea, imeanguka wakati ikitua katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa San Francisco na kuuwa watu wawili, na kujeruhi wengi.

Ndege hiyo iliyokuwa na abiria zaidi ya 300, ilipata ajali hiyo siku ya jumamosi asubuhi mara baada ya kutua katika njia yake kwa ajili ya kusima.

 Abiria 180 walikimbizwa katika hospitali zilizo karibu huku wengine wakitoka na majeraha madogo madogo.

Kutokana na maelezo ya maofisa wa shirika hilo la ndege, ajali ya ndege yaohaijatokana na tatizo la injini bali kuna tatizo lingine ambali bado halijajulikana kwa sababu hali ya hewa ilikuwa shwari kabisa.

 Kwenye mabaki ya ndege hiyo wataalamu wameweza kupata kifaa kinachoitwa Black Box ambacho hu-rekodi mambo yote ya safari ya ndege, na hivyo kusaidia kupata majibu juu ya sababu ya ajali hii.






Post a Comment

Previous Post Next Post