RAGE AWAKARIBISHA WANACHAMA WA SIMBA KATIKA MKUTANO MKUU KESHO

Mwenyekiti wa Simba SC, Aden Rage.
MWENYEKITI wa Simba, Mhe; Ismail Aden Rage, anawakaribisha wanachama wote wa Simba katika Mkutano Mkuu wa Wanachama utakaofanyika kesho katika bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Mkutano huo ni wa kawaida wa kila mwaka na unaendeleza utaratibu wa uongozi wa Alhaji Rage kufanya mikutano kama hiyo kwa kadri Katiba ya klabu inavyotaka.
Ikumbukwe kuwa katika miaka ya nyuma, kuna kipindi klabu haikuwa ikifanya mikutano kama hii kwa kipindi kirefu na hivyo huu ni utaratibu mwafaka katika kuendeleza klabu ya SIMBA.
Kwa mwaliko huu, Mwenyekiti anawataka wanachama wote walio hai kuhudhuria mkutano huo na KLABU INASISITIZA KWAMBA WANACHAMA AMBAO HAWATAKUWA HAI HADI ASUBUHI YA SIKU YA MKUTANO HAWATARUHUSIWA KUINGIA MKUTANONI. HII MAANA YAKE NI KWAMBA WANACHAMA HAWARUHUSIWI KULIPIA KADI ZAO KWENYE ENEO LA MKUTANO SIKU YA MKUTANO.
Mkutano unatarajiwa kuanza saa tatu kamili asubuhi na wanachama wote wanaombwa kujali muda.
Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo utapokea na kujadili Ripoti ya Mapato na Matumizi ya Klabu kwa mwaka ulioisha kama ilivyokaguliwa na wakaguzi wa hesabu, kupokea taarifa ya Mpango Mkakati wa Klabu (Strategic Plan) ulioandaliwa na maprofesa wa Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT).

Post a Comment

أحدث أقدم