ZIARA A RAIS JK MKOANI KAGERA

 Rais Jakaya Kikwete akitawazwa kuwa Omukama (Chifu) wa Missenyi wakati wa ziara yake ya siku sita mkoani Kagera. Anayemsimika ni kiongozi wa wazee wa Missenyi, Mzee Ernest Babeiya.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya Kyaka-Bugene kwa kiwango cha lami katika kijiji cha  Bunazi, mkoani Kagera, akiwa na mawaziri alioongozana nao katika ziara yake hiyo ya siku sita mkoani humo.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wanahabari wa vyombo mbalimbali wa mkoa wa Kagera ambao waliongozana naye katika ziara yake ya siku sita mkoani humo. Rais Kikwete amewapongeza wanahabari hao na kutoa shukurani nyingi kwa kazi nzuri ya kuufahamisha umma kila hatua ya ziara yake kwa ufasaha na weledi.

Wanahabari hao pia wamefurahi kuona kwamba Rais hakuja na jopo la wanahabari kutoka Dar es salaam kwa kuwaamini wao, hatua anbayo  wamesema imewapa faraja na furaha kubwa na  kujiamini zaidi.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya Kyaka-Bugene kwa kiwango cha lami katika kijiji cha  Bunazi, mkoani Kagera, akiwa na mawaziri alioongozana nao katika ziara yake hiyo ya siku sita mkoani humo.

Post a Comment

Previous Post Next Post