Mhe.Balozi Liberata Mulamula, Balozi wa Jamhuri ya Muungano waTanzania nchini Marekani na Mexico akiwa katika picha ya pamoja na Mhe.Charles Stith,Balozi wa zamani wa Marekani nchini Tanzania,Tanzania House,Washington DC.
Mhe.Liberata Mulamula,Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico akiwa katika picha pamoja na Mhe. Charles Stith,Balozi wa zamani wa Marekani nchi Tanzania. Kulia ni Bw.Suleiman Saleh,Afisa Ubalozi wa Tanzania Washington DC
Mhe.Liberata
Mulamula, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na
Mexico ametembelewa na aliyekuwa Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe.
Charles Stith Ubalozini Tanzania House Washington DC juzi Jumatano
Agosti 27,2013. Balozi Stith alifika Ubalozi hapo kusalimiana na Balozi
Mulamula na kumpongeza kwa kuchaguliwa kwake kushika wadhifa wake mpya
wa kuiwakilisha Tanzania nchini Marekani.
Katika
mazungumzo yao,Balozi Stith alionyesha dhamira kubwa na utayari wake
kushirikiana na Mhe.Balozi Mulamula katika kujenga mashirikiano baina
vyuo vikuu vya Marekani na vile vya Tanzania. Balozi Stith alimweleza
Balozi Mulamula kwamba anaifahamu vizuri Tanzania na ni nchi ambayo
amekuwa na mahusiano mazuri pamoja na watu wake akiwa Balozi na hadi
sasa. Kwa msingi huo, Balozi Stith alibainisha umuhimu wa kuweka mkakati
mahususi wa kukamilsha azma hiyo na kuahidi kwamba muda wowote kuanzia
sasa yupo tayari katika kutekeleza dhamira hiyo
Post a Comment