Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen, amepata gari jipya lenye
hadhi yake.
Kocha huyo raia wa Denmark, alikuwa na mikasa mingi ya magari
aliyokuwa akiyatumia, ambayo mengi yalikuwa na matatizo makubwa kiasi cha
wakati mwingine kuharibika njiani.
Mara ya mwisho alikuwa akitumia gari aina ya Rav 4, ambalo
awali lilikuwa likitumiwa na katibu mkuu wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), Frederick Mwakalebela.
Hivi karibuni, Kim amekuwa akiranda na gari hilo jipya kabisa aina ya Ford Everest lenye thamani ya Sh milioni 78, likiwa ndilo ghali zaidi kutumiwa na makocha wa nchini.
Uchunguzi uliofanywa na Championi Jumatano umebaini kwamba,
katika makocha wa klabu za ligi, anayemfuatia Kim kwa kutumia gari la gharama
ni Hemed Morocco wa Coastal Union, mwenye Land Rover Freelander linalouzwa Sh
milioni 50.
Nafasi ya tatu inashikiliwa na Kocha wa Yanga, Ernie Brandts
na yule wa Azam FC, Stewart Hall, wanaotumia magari aina ya Toyota Prado yenye
thamani ya Sh milioni 38, kila moja.
Post a Comment