Tovuti ya NairobiWire imeripoti
kuwa baadhi ya wafanyabiashara na wachuuzi katika eneo la mji mkuu wa
Nairobi, River Road na barabara nyinginezo, wameanza kuuza nakala za DVD
za shambulio la kigaidi la Jumamosi ya tarehe 21, Septemba 2013,
lililosababisha maafa makubwa nchini Kenya na kuleta simanzi katika
maeneo mbalimbali duniani.
Inawezekana kabisa ikawa ni nafasi ya kujipatia kumbukumbu lakini inashangaza kidogo uharaka wa ufyatuaji santuri hizo
kabla
ya taarifa kamili kuhusu tukio hilo haijatolewa rasmi. Inasemekana
DVDs zinazouzwa sasa katika majina tofauti (bofya picha hapo juu) ni
mkusanyiko wa taarifa mbalimbali zilizoripitiwa hadi saa kuhusu tukio
hilo. Kwa mapungufu hayo, pengine ndiyo zitatoka parts 1, 2, 3, 4 mpaka
infinity.
Najaribu kulinganisha miaka kama kumi hivi na kurudi nyuma iliyopita, hadi kwenye tukio la mwaka 1998 la kulipuliwa kwa balozi mbili za Marekani nchini Kenya na Tanzania, najiuliza kama wakati ule watu walikuwa wazubaifu wa 'kuchangamkia' fursa ya ujasiriamali katika maafa na msiba na vilio vya wengine au waliwakosesha watu kumbukumbu muhimu.
Pengine ndiyo mabadiliko ya nyakati hizi, kila jambo kama wasemavyo wenyewe, 'inategemea mtizamo wako.
Inawezekana kabisa ikawa ni nafasi ya kujipatia kumbukumbu lakini inashangaza kidogo uharaka wa ufyatuaji santuri hizo
Najaribu kulinganisha miaka kama kumi hivi na kurudi nyuma iliyopita, hadi kwenye tukio la mwaka 1998 la kulipuliwa kwa balozi mbili za Marekani nchini Kenya na Tanzania, najiuliza kama wakati ule watu walikuwa wazubaifu wa 'kuchangamkia' fursa ya ujasiriamali katika maafa na msiba na vilio vya wengine au waliwakosesha watu kumbukumbu muhimu.
Pengine ndiyo mabadiliko ya nyakati hizi, kila jambo kama wasemavyo wenyewe, 'inategemea mtizamo wako.
Post a Comment