Mahakama ya Juu nchini
Bangladesh imemhukumu kifo mwanasiasa wa kiislamu aliyepatikana na hatia
ya mauaji ya halaiki wakati wa vita vya Ukombozi kutoka kwa Pakistan
mwaka 1971.
Abdul Quader Mollah wa chama cha upinzani cha
Jamaat E Islami alihukumiwa maisha na mahakama maalum ya uhalifu wa
kivita hapo mwezi Fabruari.Hukumu ya awali ilichochea maandamano ya wafuasi wa chama chake ambao wamesema hukumu dhidi ya Mollah imechochewa kisiasa.
Lakini wapinzani wake wanasema kuwa hukumu hiyo ni dhaifu mno.
Maelfu walifanya maandamano kote nchini wakitaka Mullah ambaye alipatikana na hatia ya kuongoza mauaji ya halaiki wakati wa vita vibaya zaidi vya kupigania uhuru anyongwe.
Maandamano hayo yalichochea bunge kufanya mageuzi ya sheria ambayo yanaruhusu serikali kukata rufaa dhidi ya uamuzi wowote ulioafikiwa na mahakama maalum ya uhalifu wa kivita nchini humo.
- bbc
Post a Comment