Shahidi wa kwanza kutoka upande
wa mashtaka, amefika mbele ya mahakama ya kimataifa ICC kutoa ushahidi
dhidi ya naibu Rais wa Kenya William Ruto.
Ruto anakabiliwa na tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2007-2008
Kesi dhidi ya Ruto na mshtakiwa
mwenzake Joshua Arap Sang, ilianza tarehe 10 mwezi Septemba, baada ya
wawili hao kutuhumiwa katika kuhusika na ghasia hizo za mwaka 2007.
Kumekuwa na wasiwasi kuhusu mashahidi kujiondoa
kwenye kesi hiyo wakihofia usalama wao. Mwishoni mwa wiki, mashahidi
wanne walijiondoa katika kesi hiyo baada ya kuelezea wasiwasi kuhusu
usalama wao ikiwa watatoa ushahidi mbele ya mahakama hiyo.
Wiki jana mkuu kwenye kesi hiyo, aliakhirisha
kesi hiyo kwa sababu mashahidi hawakuwa wamefika kwenye mahakama hiyo
kutoa ushahidi wao.
Rais Uhuru Kenyatta, anatarajiwa kufik- Bofya hapa
Post a Comment