Sam akiwa studio za Defatality |
Msanii
wa muziki wa kizazi kipya Sam wa Ukweli aliyehit sana kipindi flani kwa
ngoma zake mbili ‘Sina raha’ na ‘Hata kwetu wapo’, amefunguka
exclusively kupitia bongo5 kuhusu sababu zilizompelekea huwa kimya kwa
muda mrefu na kutoyagusa tena matawi ya nyimbo hizo mbili.
Kuhusu sababu za ukimya wake na kama ameshafanya kazi kadhaa na Mensen Selekta
Jana mwimbaji huyo aliweka picha kwenye instagram akiwa katika studio za DeFatality akifanya kazi baada ya kimya kirefu .
“Hii ni mara yangu ya kwanza nafanya kazi na Mensen Selekta, na
kikubwa ambacho kilichokuwa kimenikwamisha ni kwa sababu ile management
niliyokuwa nafanya nayo kazi zamani, kuna some problems zilitokea baina
yangu mimi na wao kwa sababu kuna taratibu tulizokuwa tumepanga mimi na
wao lakini walienda kinyume na mimi kwa hiyo nikawa siwezi kusimama kwa
hiyo nikastopisha.
Sam aliendelea kusema “ Kwa hiyo swala la mkataba likawa limenibana nikawa nimeweka vikwazo kuwa siwezi kufanya kazi na mtu yeyote mpaka nimalize ule mkataba (Papaa Misifa). Kwa hiyo hivi sasa mkataba umekwisha niko huru naweza kufanya kazi na mtu yeyote na ndo maana jana nimeenda studio nikafanya kazi na Mensen Selekta, na ni kazi nzuri naamini itafanya poa.”
Sam aliendelea kusema “ Kwa hiyo swala la mkataba likawa limenibana nikawa nimeweka vikwazo kuwa siwezi kufanya kazi na mtu yeyote mpaka nimalize ule mkataba (Papaa Misifa). Kwa hiyo hivi sasa mkataba umekwisha niko huru naweza kufanya kazi na mtu yeyote na ndo maana jana nimeenda studio nikafanya kazi na Mensen Selekta, na ni kazi nzuri naamini itafanya poa.”
Kuhusu Wimbo ambao ameurekodi kwa Mensen Selekta na ujumbe wake
“Hii ni ngoma moja ambayo nimeifanya pale , na ngoma inaitwa
‘Umetumwa’ , na kitu ambacho nimezungumzia humo ndani ni kama partition
tatu tofauti. Kwanza nazungumzia kuhusu mahusiano ya watu ambayo mtu
anataka kuyaingilia japokuwa hajui wameanzia wapi, pili nimezungumzia
kuhusu Muziki kwa sababu mimi na wewe tunaweza kuwa wanamuziki halafu
akawepo mtu ambae anataka kututumia kwa kutugombanisha kwa maslahi yake
yeye lakini akatuumiza mimi na wewe ikawa mimi na wewe tunavurugana
halafu anapata mafanikio yeye. Tatu nikawa nazungumzia maisha tunayoishi
sisi inawezekana kwenye nyumba, majirani ama nyumba za kupanga
inawezekana nyie mkawa mnakaa sehemu moja na na mnaelewana halafu
ikatokea mtu akaoa mwanamke ama hata akaleta mtoto ambae akaanzisha
chokochoko kuwagombanisha nyinyi. Hata wewe unaweza kumwambia mtu ‘mi
sina ugomvi na wewe, vipi bwana umetumwa.”
Kuhusu Mahusiano yake na Producer wake ‘Kisaka’ na chanzo cha ugomvi wake na Papaa Misifa
“Kwa Kisaka nilikuwa nafanya nae kazi tu kama production, kama
marafiki na ndugu, ni mtu ambae nimefanya nae kazi kwa muda mrefu lakini
hatukuwa na mkataba wowote, na ndo maana first time nilifanya nae ‘Sina
Raha’ na ‘Hata Kwetu wapo’, project ambayo ilikuwa chini usimamizi wa
Kisaka. lakini baadae nikampata mtu anaeitwa Papaa Misifa ambae ana
kampuni ya Aljazeera Entertainment, na first time ilikuwa ikifanya kazi
na Diamond, Diana na Timbulo, so jamaa akakaa akasema tufanye kazi kwa
kuwa nina kipaji kizuri na uwezo mzuri, nikaona sawa.
Lakini sikuwa najua lengo lake, labda lengo lake lilikuwa anataka
ni-drop kwa kuwa kuna mtu ambae nilikuwa nacompete nae, ama alitaka
nipotee tu kwenye huu muziki manake mtu mwingine anaweza kuwa
anakutafuta sana akakukosa akaamua kukutafuta huku. Kwa hiyo kwenye
project yote wimbo ambao tuliufanya ni ‘Samaki’, na video pekee yake
tulizungushana takribani mwaka mzima,akawa ananiambia tayari ameshamlipa
pesa Adam wa Visual lab na kumbe uongo, kwa hiyo kulikuwa na
uongouongo, kwa hiyo lilikuwa la kwanza. La pili , tulikuwa tunafanya
show Kahama na kukawa na mazingira ya kututapeli ndo tukacomplain
tukagombanagombana lakini tukawa tumesuluhisha yakawa yameisha.
Sam aliendelea kufunguka, “Kwa hiyo ni mtu ambae anafanya vitu
ambavyo viko wrong, alikuwa anaenda Push Mobile ambapo ngoma yangu ya
‘Sina Raha’ na ‘Hata kwetu wapo’ zilikuwa zinafanya vizuri, akawa
anaenda anachukua pesa bila kunambia wakati hizo akaunti zilikuwa
hazimhusu zilikuwa zangu binafsi. Kwa hiyo nilikuwa nikipigiwa simu na
Push Mobile kuwa pesa zimetoka nikienda nakuta yeye ameshachukua. Kwa
hiyo nikaona mtu kama huyo mkifanya show mkapata hata million Ishirini
anaweza kukuletea majambazi home, kwa hiyo sio mtu mzuri kufanya nae
kazi na mimi nikamwambia bwana mimi sitaki kufanya kazi na wewe tena,
akanambia hili swala litakuwa gumu we kama unataka kuachana na mimi
subiri mpaka mkataba uishe”.
Kuhusu Project zake zinazokuja na kama atasimama mwenyewe au na manager mpya
Sasa hivi nimeamua kusimama mimi kama mimi na naandaa Project yangu
ni kama mixtape, inayoitwa “Come Back Sam wa Ukweli, Mjini Kimenuka”, na
kuna ngoma yangu ambayo nimeiachia nikiwa na Rich Mavoko na Z Anton, na
baada ya hiyo zitafuata ambazo nimefanya na maproducer mbalimbali
akiwemo Man Walter, Kwa Mazoo, Mensen Selekta, na wengine wengi yaani
nafanya na producer yoyote, niko huru.
Kuhusu alichokikosa baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu
“Kwanza kabisa namshukuru Mungu kwamba nina afya nzuri, lakini
nachojutia hasa ni kwamba watu kumiss ladha yangu kwa sababu ni mtu
ambae nina madini mengi ambayo yanataka kumwagika ila kuna watu ni kama
wameyafungia hivi.
Kitu kingine nachokijutia ni ‘Happiness’ kwa kuwa nilikuwa ni mtu
mwenye furaha naechat na watu vizuri na nini, lakini pia kukaa kimya
kwenye huu muziki kuna baadhi ya watu wako kama vile wamenisahau lakini
wadau, mashabiki muendelee kusapoti muziki wangu Sam wa ukweli
nimesimama tena upya, Mungu pekee ndiye anatakiwa aabudiwe na
kushukuriwa kwa kufanaya hadi leo mimi niko hapa”.
Post a Comment