
Nararua kama Simba; Tambwe Amisi akishangilia na Ramadhani Singano 'Messi'

MSHAMBULIAJI
mpya Mrundi wa Simba SC, Amisi Tambwe leo amefungua akaunti ya mabao
katika klabu hiyo, baada ya kufunga mawili katika ushindi wa 4-3 dhidi
ya Mafunzo ya Zanzibar katika mchezo wa kirafiki uliofanyika kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii.
Pamoja
na kufunga mabao mawili, Tambwe pia alitoa pasi ya bao la pili- hivyo
kuwaonyesha Simba SC kwamba hawakukosea kumsajili.
Mchezaji
huyo kutoka Vital’O ya Burundi na mfungaji bora wa Klabu Afrika
Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mwaka huu, aling’ara katika mchezo wa
leo sawa na beki Kaze Gilbert waliyesajiliwa naye wote kutoka Vital’O.
Hadi
mapumziko, tayari timu hizo zilikuwa zimekwishafungana bao 1-1, Mafunzo
wakitangulia kupitia kwa Ally Juma dakika ya 32 na Amisi Tambwe
akiisawazishia Simba SC dakika ya 45.
Mafunzo
walipata bao lao kwa shuti la mpira wa adhabu kutoka upande wa kulia wa
Uwanja umbali wa mita 24, lililomshinda kipa Andrew Ntalla na kutinga
nyavuni.
Simba
ilisawazisha baada ya Tambwe kuuwahi mpira uliorudi baada ya kugonga
mwamba kufuatia yeye mwenyewe kupiga kichwa akiunganisha krosi ya Rashid
Ismail kutoka upande wa kulia wa Uwanja.
Kipindi
cha pili, Simba SC iliingia na moto na kufanikiwa kupata bao la pili
dakika ya 47 tu mfungaji Sino Augustino aliyeingia kipindi cha pili
kuchukua nafasi ya Rashid Ismail kwa shuti kali baada ya kupokea pasi ya
Amisi Tambwe.
Mafunzo
ilisawazisha bao hilo dakika ya 52 mfungaji Jaku Juma aliyeunganisha
pasi nzuri ya Ally Juma baada ya mabeki wa Simba SC kuchanganyana.
Dakika
ya 72, Juma Jaku aliifungia Mafunzo bao la tatu, akiunganisha krosi ya
Heri Salum ikiwa ni dakika moja tu tangu kipa Abbel Dhaira aingie
kuchukua nafasi ya Andrew Ntalla.
Tambwe aliifungia Simba SC bao la kusawazisaha dakika ya 81, akiunganisha krosi ya Nassor Masoud ‘Chollo’.
Nahodha
Nassor Masoud ‘Chollo’ aliifungia Simba SC bao la nne dakika ya 83
baada ya gonga safi, mpira ukianzia kwa Ramadhani Singano ‘Messi’
aliyempa Said Ndemla ambaye akampasia mfungaji aliyewainua vitini wana
Msimbazi.
Simba
SC; Anderw Ntalla/Abbel Dhaira, Nassor Masoud ‘Chollo’, Issa Rashid
‘Baba Ubaya’, Miraj Adam, Gilbert Kaze, Abdulhalim Humud
‘Gaucho’/William Lucian ‘Gallas’, Ramadhani Singano ‘Messi’, Said
Ndemla, Amisi Tambwe, Rashid Ismail/Sino Augustino na Ramadhani Chombo
‘Redondo’/Zahor Pazi.
Mafunzo; Abdul Suleiman, Hamadi Hajji/Hajji Abdi, Abdul Abdallah, Heri Salum, Said Mussa, Juma Othman/Haji Mwambe, Mohamed Abdul, Masoud Hamad/Wahid Ibrahim, Juma Jaku, Ally Othman/Sadick Habib na Ally Juma.
![]() |
Salamu zenu Jangwani; Tambwe Amisi leo amefungua akaunti ya mabao Simba SC |
Mafunzo; Abdul Suleiman, Hamadi Hajji/Hajji Abdi, Abdul Abdallah, Heri Salum, Said Mussa, Juma Othman/Haji Mwambe, Mohamed Abdul, Masoud Hamad/Wahid Ibrahim, Juma Jaku, Ally Othman/Sadick Habib na Ally Juma.
إرسال تعليق