Raisi wa Msumbiji Armando Guebuza kufanya mazungumzo na chama cha Renamo ili kunusuru amani ya Msumbiji/bbc.co.uk
|
Na Martha Saranga Amini
Rais wa Msumbiji Armando Guebuza ameomba nafasi ya kufanya mazungumzo na
lililokuwa kundi la waasi la Renamo ambalo sasa linatambuliwa kama
chama cha siasa.
Rais Guebuza amesema wanahitaji kutafuta suluhu la haraka ili kulinda amani ya nchi hiyo ambayo kwa sasa imetetereka.
Ombi hilo linakuja baada ya ghasia za hivi karibuni baina ya vikosi vya
serikali na Renamo, walitangaza kusitisha kuutambua mkataba wa amani wa
mwaka 1992 uliotamatisha machafuko yaliyodumu kwa miaka 16.
Uhusiano baina ya chama tawala cha Frelimo na wapinzani wa Renamo
umekuwa tete katika siku za hivi karibuni, huku mataifa mbalimbali na
jumuiya ya kimataifa ikitoa wito kwa pande hizo mbili kumaliza tofauti
zao kwa mazungumzo ili kuepusha umwagaji damu.
Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa UN, Ban Ki-moon alitoa wito
alhamisi kwa serikali ya Msumbiji pamoja na lililokuwa kundi la waasi
nchini humo Renamo kufanya mazungumzo sambamba na kuepuka ghasia
zinazohatarisha amani na usalama nchini humo.
Siku kadhaa baada ya Renamo kusitisha kuutambua mkataba wa amani wa
mwaka 1992 uliomaliza machafuko ya miaka 16, hofu ya kutumbukia katika
mapigano ya wenyewe kwa wenyewe imezidi kutanda nchini humo.
Shule zimeripotiwa kufungwa katika maeneo yanayoizunguka kambi ya Renamo
kutokana na hofu ya usalama, huku mataifa kama Marekani yakizidi
kuhimiza pande zote kumaliza tofauti zao.
Nao Ubalozi wa Ufaransa mjini Maputo umeonya dhidi ya raia wake waishio
nchini humo kutosafiri kuelekea katika jimbo la Sofala ambalo ni kitovu
cha machafuko baina ya Renamo na vikosi vya serikali.
Via kiswahili.rfi.fr
Post a Comment