Unapotazama video za msanii wa Genge maarufu kama Mejja kutoka
Kenya, utagundua kwamba utamu wa muziki wake unapatikana zaidi katika
video kuliko unaposikiliza kwenye radio peke yake, kwasababu amejaaliwa
kipaji cha kuchekesha kuanzia unapomtazama sura yake tu yuko ki comedy
sana.
Mejja ameamua kufuata ushauri wa mashabiki wake waliokuwa wakimshauri
kuanza kufanya comedy sababu ameonekana kuwa comedian mzuri kupitia
video za nyimbo zake zikiwemo Land Lord, Jana kuliendaje, Raundi hii si
mchezo za nyingine alizoshirikishwa na Jua Cali.
Akizungumza katika mahojiano na Milele FM ya Kenya, Meme Hadhija aka
Mejja ambaye yuko chini ya Calif Records amesema anakubali kuwa
anakipaji cha kuchekesha na anatarajia kuanza kurekodi video za comedy
na kuziweka youtube kwaajili ya mashabiki wake.
Tazama video ya wimbo wake ‘Landlord’ ucheke kidogo!
Post a Comment