Nay wa Mitego amefunguka na kusema kuwa anatarajia kutoa wimbo mpya uitwao ‘Nakula Ujana’ ili kuwaonesha watu kuwa habahatishi.
Akizungumza jana, Nay alisema kumekuwa na mitazamo tofauti
kutoka kwa watu kwamba yeye hubahatisha kwenye muziki na hivyo anataka
kuwaonesha tofauti.
“Unajua nafanya muziki kwa uwezo wangu ndio maana tarehe 20 mwezi
huu naachia wimbo mpya ambao kiukweli naamini utafanya vizuri. Muziki
Gani watu walisema Diamond alisaidia ile ngoma kufanya poa,lakini
kiukweli wimbo ulikuwa ni mzuri ndio maana ukafanya poa,” alisema Nay.
“Wimbo unaofuata utakuwa una ladha tofauti kwasababu kuna uimbaji wa
tofauti ambao nimeufanya katika wimbo wangu ‘Nakula Ujana’ ili kupata
ladha tofauti, ambayo naimani itafanya poa, na pia sipendi kukaa muda
mrefu bila kufanya ngoma.”
Post a Comment