Rais Kikwete akisalimiana na
Mwambata wa Kijeshi katika Ubalozi wa Tanzania Afrika kusini katika
uwanja wa ndege wa Waterkloof Airforce Base ulioko Kusini mwa jiji la
Pretoria. (picha hii na zilizopachikwa hapo chini ni kutoka Ikulu)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili katika mji mkuu wa
Afrika Kusini wa Pretoria usiku wa leo, Jumatatu, Desemba 9, 2013,
kuhudhuria Ibada Kuu ya Kitaifa (Memorial Service) ya msiba wa Rais
Mstaafu wa Afrika Kusini Mzee Nelson R. Mandela kwenye Uwanja wa
Michezo wa FNB mjini Johannesburg.
Rais Kikwete anajiunga na mamia ya viongozi wa nchi mbali mbali duniani kuomboleza kifo cha mmoja wa
Rais Kikwete anajiunga na mamia ya viongozi wa nchi mbali mbali duniani kuomboleza kifo cha mmoja wa
viongozi mashuhuri zaidi duniani katika karne za 20 na 21.
Rais Kikwete ameambatana na Makamu Mwenyekiti wa Pili wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd na mkewe Mama Asha; Mama Salma Kikwete na Ndugu Abdulahramani Kinana, Katibu wa Mkuu wa CCM.
Rais Kikwete ameambatana na Makamu Mwenyekiti wa Pili wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd na mkewe Mama Asha; Mama Salma Kikwete na Ndugu Abdulahramani Kinana, Katibu wa Mkuu wa CCM.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete
akilakiwa katika uwanja wa ndege wa Waterkloof Airforce Base ulioko
Kusini mwa jiji la Pretoria alikowasili usiku wa kuamkia leo tayari
kuhudhuria mazishi ya Rais Mstaafu wa Afrika Kusini Mzee Nelson R.
Mandela.
Rais Kikwete akisindikizwa
kuelekea kwenye gari baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Waterkloof
Airforce Base ulioko Kusini mwa jiji la Pretoria . Nyuma yake mwenye
ushungi kichwani ni Mama Salma Kikwete
Rais Kikwete akisindikizwa
kuelekea kwenye gari baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Waterkloof
Airforce Base ulioko Kusini mwa jiji la Pretoria . Nyuma yake kushoto ni
Katibu Mkuu wa CCM Ndg Abdurahman Kinana.
إرسال تعليق