ARSENAL YASHINDA 2 - 1, YAREJEA KILELENI LIGI KUU ENGLAND

SI mchezo, Ligi Kuu ya England mwaka huu ni shughuli pevu. Jumamosi, Chelsea alikuwa kileleni, Jumapili, Manchester City na sasa ni Arsenal. Kiasi cha pointi mbili tu kinazitenganisha timu tatu za juu.
Kikosi cha Arsene Wenger kimerejea kileleni kufuatia ushindi wa mabao 2-1 ugenini usiku huu dhidi ya Aston Villa. Jack Wilshere alifunga dakika ya 34 na Olivier Giroud akafunga la pili dakika ya 35 Arsenal ikaongoza 2-0 kabla ya Cristian Benteke kuifungia Villa la kufutia machozi dakika ya 76.
Arsenal inarejea kileleni kwa pointi zake 48, ikiishusha Manchester City yenye pointi 47 katika nafasi ya pili, mbele ya Chelsea yenye pointi 46.

Tabasamu kileleni: Olivier Giroud akishangilia na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao la pili

Post a Comment

أحدث أقدم