Papa Francis adai internet ni zawadi kutoka kwa Mungu

Papa Francis2Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesema kuwa Internet ni zawadi kwa dunia nzima kutoka kwa Mungu lakini akaonya kuwa matamanio ya kutaka kuwasiliana zaidi kutumia Internet kunawatenga watu kutoka kwa familia na marafiki zao.
Amewataka waumuni wa kikatoliki kujiunga na mfumo wa dijitali. “Internet… inatoa nafasi ya mafanikio mengi. “Hiki ni kitu kizuri bila shaka ni zawadi kutoka kwa Mungu,” alisema Papa.
Katika ujumbe wake kwa dunia nzima ambao hutolewa kila mwaka, Papa amesema kuwa mfumo wa dijitali, unapaswa kuwa mtandao wa watu wala sio nyaya tupu.
Amehimiza kuwa mawasiliano yanapaswa kuhusisha hisia na mawazo, watu kukutana na kujuliana hali,huku akiwataka waumini wa kikatoliki kutodhani kuwa ni mawazo yao na imani zao pekee ambazo ni muhimu wakati wakiwasiliana na watu wa dini nyinginezo.
Papa ana akaunti kwenye mitandao ya Twitter na Facebook ambayo ina wafuasi zaidi ya milioni wengi.
Source:BBC

Post a Comment

Previous Post Next Post